TAARIFA KWA UMMA KUHUSU BEI ZA MAFUTA KATIKA SOKO LA DUNIA NA LA HAPA NCHINI

Mamlaka ya Huduma za Nishati na Maji (EWURA) inapenda kutoa taarifa halisi kuhusiana na mwenendo wa bei za mafuta katika soko la dunia na la hapa nchini. Kati ya majukumu ambayo EWURA imepewa ni kuweka bei KIKOMO za mafuta aina ya petroli katika soko la hapa nchini, utaratibu ulioanza rasmi Januari 6, mwaka 2009 baada ya kutokea hali ya kukosekana uhalisia wa bei za mafuta katika soko la ndani ikilinganishwa na mwenendo wa bei katika soko la dunia. Matokeo yake ni kuwa watumiaji mafuta walikuwa wakinunua mafuta kwa bei isiyo halisi (2,200/= kwa lita) katika miezi ya mwisho mwaka 2008, na pia uchumi wa nchi uliathirika na mwenendo huu wa bei. EWURA ilishusha bei hizo hadi kufikia 1,140/= baada ya kuanza kupanga bei mwezi Januari 2009.

Attachment; Taarifa kwa umma kuhusu bei za mafuta katika soko la dunia na la hapa nchini

Visits: 362