TANGAZO: Majina ya Waombaji wa Leseni za Umeme Waliopitishwa na Bodi Kupewa Leseni Tarehe 22/6/2019

Kwa tangazo hili, waombaji hawa wanatakiwa kuwasiliana na ofisi za EWURA Makao Makuu – Dodoma au Ofisi za Kanda ili kupata Control Number kwa ajili ya kulipia ada za leseni na kuchukua leseni zao. Soma Zaidi:-Orodha ya Wakandarasi Waliopitishwa kupewa Leseni-22062019

 

Hits: 4739

125 thoughts on “TANGAZO: Majina ya Waombaji wa Leseni za Umeme Waliopitishwa na Bodi Kupewa Leseni Tarehe 22/6/2019

    1. Ndugu Mbwago,
      Fanya maombi kupitia mtandao wa intaneti. Bofya kiunganishi Online Services katika tovuti yetu na kisha bofya LOIS kujisajili.
      Hakikisha una nakala ya vyeti vyako zilizothibitishwa, picha ya pasipoti yenye kivuli cha bluu na wasifu wako (CV). Vyote hivi viwe katika nakala laini ili uweze kuvitumia unapofanya maombi mtandaoni.
      Kwa maelezo zaidi piga 0800110030.
      Karibu

      1. Naomba kujua mm niliomba leseni 2018 September, December nikaitwa Mwanza ili nikailipie nakuchukua ,sikukua Mwanza hinyo sikuweza kuichukua nitumie utaratbu upi ili niipate

        1. Ndugu Yona,
          Fika ofisi yetu ya Mwanza ili uweze kuchukua leseni yako.
          Unaweza pia kupiga simu bure 0800110030 ili kuunganishwa na Afisa wetu wa Mwanza anayeshughulikia masuala ya leseni.
          Ofisi yetu ya Kanda ya Ziwa ipo Ghorofa ya 4,Upande wa Mbele,PPF Plaza, Barabara Kenyatta,S.L.P 2069, Mwanza, TanzaniaSimu:+255 28 2506071-72; Nukushi +255 28 2506073

          1. Mimi nifundi Nina elimu ya mwaka wa pili level two nimetuma maombi ya leseni nikaweka cheti cha level two yani cha baraza la mitihani Veta (vc2),cheti cha kuzaliwa na passport size,na mfumo ukapokea maombi je kulikua na umuhimu wa kuweka leaving ya veta

      2. Mimi ni shadrack shida yangu kila ninapo ingia mtandaoni kwaajili ya ujazaji form inagoma kuna kuwa na shida gani ?

        1. Habari Shadrack,
          Pole kwa changamoto.
          Tafadhali naomba kufahamu upo wapi na tupatie namba yako ya simu.
          Unaweza pia kupiga simu bure 0800110030 ili kutatuliwa suala lako.

        2. Ndugu Shdrack, pole sana.
          Tafadhali piga simu 0800110030 (bure) ili suala lako lifanyiwe kazi zaidi.
          Karibu

    2. Mimi ni james sanga nili omba maombi ya kuhuwisha lesseni yangu mwaka jana (Mwanza) mpaka leo sijapata JAMES SANGAELINC/2019/3481

  1. Nauliza kuhusu hizo leseni za Electrical Installation; nilipata taarifa hizi kupitia kwenye maonesho ya sabasab kupitia TV nikapata anwani ya email hii ila nimeshidwa wap haswa ndio kuna hizo process za kujiunga ili kuweza kupata hivyo leseni kwa sababu mm ni mwanafunzi nlio hitimu katk fani hiyo kwa miaka mitatu kutoka hapa RVTSC MOSHI (Veta Moshi) na punde nasubiria matokeo yangu ya mwaka wa tatu. Katika utafutaji wa rizq basi sharti utii vigezo na masharti bila kushurutishwa naomba kujiunga katika upewaji wa leseni na vipi taratibu zake ili kuipata hiyo leseni.

  2. Mimi ni mwanafunzi nliehitimu toka Veta Moshi katika fani hiyo ya Electrical Installation kwa muda wa miaka 3 naulizia taratibu za kufanya au kujiunga kuweza kuwa na leseni ya ufundi umeme.

    1. Habari Khalidi,
      Maombi ya leseni za shughuli za ufungaji umeme hufanywa kwa njia ya mtandao kupitia https://lois.ewura.go.tz/ewura/.
      Unatakiwa kuwa na nakala laini (soft copy) za vyeti vyako, picha yenye kivuli cha bluu, wasifu wako (CV)na vyote viwe vimethibitishwa na wakili au hakimu.
      Kisha inigia katika mfumo kupitia website yetu na uendelee kujisajili na kujaza fomu.
      Unaweza pia kuwasiliana nasi bure kupitia 0800110030.
      Asante

      1. Mimi ni zeid khamis Nassoro nipo geita nifundi mzoefu wa kufunga umeme majumbani nina miaka 8 kwenye ufundi nifanyeje ili nipate resend ya ufundi

    1. Bwana Joseph,
      Mwombaji wa leseni anapaswa kuwa na elimu ya ufundi wa umeme kuanzia wiremen na kuendelea.
      Maombi ya leseni hufanywa kupitia kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/
      Unapaswa kuwa na vyeti, picha ya passport yenye kivuli cha bluu na wasifu wako-vyote vikiwa katika nakala laini kabla ya kuanza kufanya maombi.
      Unaweza kuwasilasiliana nasi zaidi bure 0800110030
      Asante

    2. Bwana Joseph,
      Mwombaji wa leseni anapaswa kuwa na elimu ya umeme kuanzia ngazi ya cheti.
      Maombi ya leseni hufanyika kwa njia ya mtandao kupitia kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/
      Unapaswa kuwa na vyeti vilivyothibitishwa, wasifu wako (CV) na picha ya pasipoti yenye kivuli cha bluu, vyote vikiwa katika nakala laini.
      Kwa msaada zaidi piga 0800110030
      Karibu

        1. Ndugu Anold,
          Leseni hutolewa ndani ya siku 30 tangu kupokelewa kwa maombi yaliyokamilika. Maombi yaliykamilika ni yale ambayo hayana marekebisho yoyote. Hivyo unashauriwa kutizama katika akaunti yako mara kwa mara kujiridhisha endapo kuna jambo lolote la kurekebisha kutoka kwetu. Pia, unaweza kupiga simu 0800110030 kwa siku za kazi kwa ufafanuzi wa suala lolote.
          Karibu

    1. Ndugu Kinunda,
      Karibu katika Ofisi yetu ya Dodoma, ghorofa ya 5 jengo la PSSSF, lilipo barabara ya Makole.
      Unaweza pia kupiga simu kupitia 0800110030 kwa maelezo zaidi.

        1. Bwana Kinunda,
          Pole, tunaomba kufahamu upo mkoa gani? Pia tuma reference number yako uliyopata kupitia LOIS.
          Asante

  3. Naomba kufahamu, toka mwaka Jana 2019 mwezi wa 7 nilituma maombi ya leseni ya ufundi Umeme. Ila mpaka mda huu sijapewa mrejesho wowote na siku nazo zinazidi kwenda. Naomba msaada kwa hili FREDY BONIPHACE MAKOYE

    1. Habari Fredy,
      Samahani naomba kufahamu upo sehemu gani na namba yako ya simu.
      Unaweza pia kupiga simu bure 0800110030.
      Asante

    1. Ndugu Emmanuel,

      Tafadhali jedwali lipo LICENCE FEE
      Type / Class of
      Licence
      Renewal Annual
      Fee (TZS)
      Initial licence
      fee
      Duplicate Licences fees
      A, S1 100,000 / – 150,000 30,000
      B, S2 80,000 / – 120,000 25,000
      C, S3 60,000 / – 100,000 20,000
      D 30,000 / – 60,000 15000
      W 20,000 / – 40,000 10,000
      Application – 10,000

      Zaidi soma kanuni “The-Electricity-Electrical-Installation-Services-Rules-2019-GN-382” inapatikana katika kiunganishi https://www.ewura.go.tz/wp-content/uploads/2019/06/The-Electricity-Electrical-Installation-Services-Rules-2019-GN-382.pdf
      Endapo utakuwa na maswali zaidi piga simu 0800110030 (bure)

  4. Naitwa Joseph Ishasi mwenye Leseni namba ENLINC-2018-1610-D. Muda wa kufanya marekebisho ya Leseni yangu umekaribia, hivyo nilikuwa nahitaji msaada wa utaratibu wa kufanya Jambo hilo.

  5. Hadi sasa ninamiez minne sijapata lesen yangu ya umeme hiv inachukua muda gani….Bernard benjamini ngonyani

    1. Bwana Bernad,pole sana
      Tafadhali tungependa kujua ulipo,namba yako ya simu ili tuweze kuwasiliana zaidi na kufanya ufuatiliaji. Unaweza kupiga simu 0800110030 (Bure) ili kuwasilisha suala lako.
      Karibu

        1. Bwana Abel,
          Leseni zote zilizokamilika hutolewa kila mwezi baada ya kupitishwa na Bodi.
          Endapo uliomba leseni na hujasikikia kutoka kwetu, tafadhali tuma Reference Number yako, Mahali ulipo na namba yako ya simu.
          Pia unaweza kufanya ufuatiliaji wa maendeleo ya leseni yako kupitia mfumo wa LOIS.
          Zaidi piga simu 0800110030 (bure) muda wa kazi.
          Karibu

  6. Habari naomba kuuliza katika progress katika Lois Ewura nimekuta ELC meeting preparation and recommended nini kinaendelea naomba kufahamishwa.

    1. Bwana Juma,
      Asante kwa mrejesho. Tutarejea kwako.
      Pia unaweza kupiga simu bure 0800110030 muda wa kazi.
      Karibu

  7. Mimi james sanga bado sijajibiwa ombi langu karibu wiki ya pili sasa.Mimi nili omba kuhuisha leseni yangu mwaka jana nikapewa namba James sanga ELNIC 2019 3481 lakini tangu mwaka jana mpaka leo sijapata kitu.Kwani kulinew inachukuaje mda mrefu hivi.MIMI NAIPENDA NCHI YANGU NILIPIE KODI.JE MIMI MTEJA WENU EWURA NIFANYEJE?

      1. Nashukulu kwa kuliona ombi langu.Ushauli wangu natamani sana light kama mafundi umememe wote wangelipata leseni.Hata serikali yetu ingenufaika na kodi,mafundi tupo wengi sana lakini wenye reseni hata robo hawafiki.Tafuteni mbinu ili kuwafikia wote.Kama BRELLA.

  8. Nashukulu kwa kuliona ombi langu.Ushauli wangu natamani sana light kama mafundi umememe wote wangelipata leseni.Hata serikali yetu ingenufaika na kodi,mafundi tupo wengi sana lakini wenye reseni hata robo hawafiki.Tafuteni mbinu ili kuwafikia wote.Kama BRELLA.

        1. Habari Bwana Mohamed,
          Kwa utaratibu wa EWURA, leseni za umeme hutolewa ndani ya siku 30 tangu kupokea maombi yaliyokamilika. Hata hivyo , ni lazima EWURA ipate uthibitisho kutoka katika chuo ulichosoma. Endapo uthibitihso utachelewa kutufikia, inaweza kupelekea leseni kuchelewa kidogo. EWURA imekuwa ikiwasiliana mara kwa mara na vyuo husika ili kuhakikisha zoezi linakamilika mapema iwezekanavyo.
          Aidha, mfumo wa LOIS huoa taarifa kwa muombaji,hivyo unashauriwa kutembelea barua yako mara kwa mara.
          Karibu

          1. Hatua gani hua mnachukua. Mbadala inapotokea ucheleweshwaji wa lipot kutoka chuo husika kwa lengo la kutusaidia wateja wenu au nini kifanyike

  9. Naitwa Raymond ,nimesoma chuo cha bugisi veta shinya , course ya electrical installation Short course chini ya usimamizi wa don Bosco pamoja na serikali,lakini nimesoma topic muhimu za electrical installation,je lesseni yangu inagharimu kiasi gani cha pesa?

    1. Ndugu Raymond,
      Gharama ya maombi ya leseni ni shilingi 10,000/
      Na malipo ya leseni ya yanategemea na aina ya leseni Wiremen sh. 20,000/;D sh 30,000/;C,S3 sh.60,000/; B,S2 sh. 80,000/ na A,S1 sh.100,000/.
      Gharama hizi ni zinadumu kwa muda wa miaka mitatu.
      Karibu

  10. Habari.Je?Mnawasaidiaje wale mafundi wa muda mrefu ambao hawana vyeti vya ufundi ila ni wabobezi ili nao wapate leseni wapate kuchangia pato la taifa?

    1. Ndugu Gilbert,
      Unapaswa kurasimisha ujuzi wako kupitia program mbalimbali ambazo hutangazwa na Serikali. Unashauriwa kufanya ufuatiliaji wa matangazo yanayotolewa mara kwa mara na Serikali ili uweze kushiriki. Vilevile unaweza kuwasiliana VETA iliyokaribu nawe huwa wana utaratibu wa kurasimisha ujuzi.
      Karibu

  11. Naitwa Sylvanus Simeo Mushumbusi.

    Nipo Dar Es Salaam,nilishafanya maombi ya leseni tayari lakini mpaka leo sijajua kinachoendelea.
    Naomba nijue inachukua muda gani!

    1. Ndugu Sylvanus,
      Ulipaswa uwe umeshapata leseni yako.
      Tafadhali tupatie namba yako ya simu kwa ufuatiliaji zaidi.
      Karibu

    1. Ndugu Shafii,
      Ofisi za EWURA Kanda ya Mashariki zipo ghorofa ya 7, jengo la PSSSF Kijitonyama,mkabala na Kijiji cha Makumbusho.
      Karibu

  12. Nimemaliza mafunzo ya ngazi ya tatu (level three) kwenye kada ya electrical installation Mwanza RVTSC,
    Je nalusiwa kupata leseni ya ewura???

    1. Ndugu Godlove,
      Ndio unaruhusiwa kupata leseni. Fanya maombi kwa njia ya mtandao kupitia LOIS inayopatikana katika tovuti yetu. Unapaswa kuwa na cheti,kitambulisho, wasifu wako(CV) na picha yenye kivuli cha bluu.
      Karibu

  13. Mimi niliomba kuuhisha lecen yangu kwani imeisha tangu tarehe 27/12/2020 na nimeiona board imekaa tarehe moja je nitaipata lini hiyo lecen ?

  14. Mimi niliomba kuuhisha lecen yangu kwani imeisha tangu tarehe 27/12/2020 na nimeiona board imekaa tarehe moja je nitaipata lini hiyo lecen ? Tarehe 1/01/2021 ndio board imekaa.

  15. Mm ni simion c simion tokea nimefanya maomb kwa njia ya mtandao toka tarehe 10/2/2021 mpaka leo bado sijapata majibu nn kinaendelea maana kila nikiingia nakuta : certificate pending na view pending naomben mnisaidie na pale niliandikiwa inachukua siku tano sas na sku zimepita Zaid ya 25

    1. Bwana Simion,
      Leseni hutolewa ndani ya siku 30 tangu kupokelewa maombi kamili. Bila shaka utakuwa umepata leseni yako ipasavyo. Endapo hujapokea leseni mpaka sasahivi, tafadhali tupatie namba yako ya simu au piga simu BURE 0800110030 siku na muda wa kazi kwa ufuatiliaji zaidi.
      Karibu

    1. Karibu Bwana Sweetbert,
      Maombi ya leseni hufanyika kwa nyia ya mtandao kupitia mfumo wa LOIS kwa kutumia kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/.
      Viambatisho vinavyotakiwa ni picha zenye kivuli cha bluu, cheti cha ufundi ,kitambulisho cha kura, taifa au leseni ya udereva na wasifu katika nakala laini.
      Kwa maelezo zaidi unaweza kupiga simu BURE 0800110030 siku na muda wa kazi au kutembelea ofisi zetu za Kanda za Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya, Mwanza na Arusha.
      Karibu

    1. Ndugu Thadey,
      Tupe muda tufuatilie, utajibiwa kuhusu suala lako. Tafadhali unaweza pia kutupatia namba yako ya simu.
      Karibu

    1. Ndugu Selemani,
      Tafadhali tufahamishe umeomba leseni ukiwa mkoa gani na utupatie namba zako za simu kwa mawasiliano zaidi. Aidha, unaweza kupiga simu bure 0800110030 muda wa kazi au kutembelea moja ya ofisi zetu iliyo karibu nawe. Ofisi za Kanda zipo Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya, Arusha na Mwanza.
      Karibu

  16. Ukitaka kuwa na leseni mpaka uwe na cheti cha veta. Je kama mtu anacho cheti cha chuo hawezi kupata au inakuaje.

    1. Ndugu Thomas,
      Ingia katika LOIS weka jina na nywila yako (pass word). Unaweza kupiga simu BURE 0800110030 siku na muda wa kazi.
      Karibu

  17. Francis frank wa korogwe, tanga niliitwa kuchukua leseni mwaka 2019 sikuweza kufika nilitoka nje nchi nimeludi je?nawezakuja kuichukua? Phone0672824572

    1. Ndugu Osten, hakuana leseni inayotolewa kwa muda mrefu kama ulivyoeleza. Tafadhali tujulishe uliomba leseni ukiwa wapi na namba yako ya simu kwa ufuatiliaji zaidi.
      Karibu.

  18. Habari Ewura. Nilipata taarifa kuwa leseni yangu iko tayari hivyo nifanye malipo na control namba yangu itaisha muda wake mwezi may mwakani. Je naweza kufanya malipo kwa awamu mbili kabla control yangu haijaisha muda wake?

  19. Ndugu Ewura nilipenda kuugana na shelia zenu kukamilisha usalama wa kazi ivo basi nilikuwa naomba resene kwausalama wakazi yagu pia nasheria kiujumula

    1. Ndugu Abednego,
      Karibu.
      Maombi ya leseni hufanyika kwa njia ya mtandao kupitia LOIS. Tafadhali bofya https://lois.ewura.go.tz/ewura/ kujisajili na kuendelea kujaza fomu ya maombi.
      Endapo utapata changamoto yoyote tupigie 0800110030 muda na siku za kazi au fika ofisi yetu iliyo karibu nawe.
      Asante

  20. Mm nipo dar es salaam Nina fanya kazi za UMEME wa majumba nn mwaka wa Tano Sasa.. ninauzoefu wa kutosha .. Sasa naomba nipate mwongozo wa kupata Lesen ya Umeme.
    Nina nyalaka zote zinazohtajika

    1. Ndugu Masoud,
      Maombi ya leseni hufanyika kwa njia ya mtandao kwa kubofya neno LOIS kwenye tovuti yetu.
      Kisha jisajili na uendelee kujaza fomu husika. Hakikisha una viambatisho ambavyo ni picha (yenye kivuki cha bluu), nakala ya vyeti vya ufundi na wasifu wako (CV). Gharama ya maombi ya leseni ni shilingi 10,000/ na hulipwa kupitia Control Number ambayo utaipata kwenye mfumo wa maombi.
      Karibu.

      1. Naomba kujuwa maendeleo ya leseni yangu ya umeme niliomba mwezi wa NNE(4) na je, ntaipata lini

    1. Ndugu Mohammed,
      Ifuatayo ni Madaraja ya leseni, elimu na mipaka ya shughuli zao.

      Daraja A Inatolewa ili kuweza kufanya kazi za ufungaji wa mifumo ya umeme katika msongo wa umeme wa aina zote. Isipokuwa hataruhusiwa kufanya kazi yoyote iliyo chini ya leseni maalumu (S1, S2 na S3) pasipokuwa na leseni husika (i) Cheti cha Usajili cha Utaalamu wa Uhandisi wa Umeme na vyeti husika vya elimu;

      (ii) Shahada ya uhandisi wa umeme au uhandisi wa umeme-mitambo au Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi ngazi ya 8 au zaidi na miaka mitatu ya uzoefu katika masuala ya kazi za kufunga mifumo ya umeme,mwaka mmoja kati ya hiyo iwe ya ufungaji wa mifumo ya umeme kwenye msongo wa juu;
      (iii) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 7 au Stashahada ya Juu ya Uhandisi wa Umeme au Umeme-mitambo na
      miaka mine ya uzoefu katika masuala ya kazi za kufunga mifumo ya umeme, miwili kati ya hiyo,iwe ya ufungaji umeme katika msongo wa juu;
      (iv) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 6 au Cheti cha Ufundi sanifu katika masuala ya uhandisi wa umeme/umeme-mitambo na miaka mitano ya uzoefu katika masuala ya kazi za kufunga mifumo ya umeme, miaka mitatu kati ya hiyo iwe ya ufungaji mifumo ya umeme wa msongo wa juu.
      Daraja B Inatolewa ili kuweza kufanya kazi za ufungaji wa mifumo ya umeme katika msongo wa kati mpaka kiasi cha msongo wa volti 33,000. Isipokuwa hataruhusiwa kufanya kazi yoyote iliyo chini ya leseni maalumu (S1, S2 na S3) pasipokuwa na leseni husika (i) Shahada ya Uhandisi wa umeme au
      uhandisi wa Umeme-Mitambo au Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi ngazi ya 8, au zaidi na miaka miwili ya uzoefu katika masuala ya kazi za kufungaji mifumo ya umeme, mwaka mmoja kati ya hiyo uwe wa ufungaji wa umeme katika msongo wa kati;
      (ii) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi ngazi ya 7 au Stashahada ya Juu ya Uhandisi wa Umeme/ Umeme-Mitambo na miaka mitatu ya uzoefu katika masuala ya kazi za kufunga mifumo ya umeme, mwaka mmoja na nusu kati ya hiyo iwe ya ufungaji umeme wa msongo wa kati; na
      (iii) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 6 au
      Cheti cha Ufundi sanifu katika masuala ya uhandisi wa umeme/ umeme- mitambo na miaka minne ya uzoefu katika masuala ya kazi za kufunga wa mifumo ya umeme, miaka miwili kati ya hiyo iwe ya ufungaji wa umeme wa msongo wa kati.
      Daraja C Inatolewa ili kuweza kufanya kazi za ufungaji wa mifumo ya umeme katika msongo usiyozidi volti 1000. isipokuwa hataruhusiwa kufanya kazi yoyote iliyo chini ya leseni maalumu (S1, S2 na S3) pasipokuwa na leseni husika (i) Shahada ya Uhandisi wa umeme/umeme-mitambo au Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi ngazi ya 8 au inayolingana na Shahada ya Uhandisi wa umeme;
      (ii) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 7 au Stashahada ya Juu ya Uhandisi wa Umeme/ Umeme-Mitambo au inayolingana na hiyo;
      (iii) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 6 au Stashahada ya kawaida ya Uhandisi wa Umeme/U meme-Mitambo au Cheti cha Ufundi sanifu katika masuala ya Uhandisi Umeme au inayolingana na hiyo katika ufungaji mifumo ya umeme,
      (iv) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi ngazi ya 4, Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi ngazi ya 5, au cheti cha kufuzu Mtihani wa ujuzi wa umeme daraja la I / Ngazi ya III au inayolingana na hiyo na miaka miwili ya uzoefu katika masuala ya kazi za kufunga mifumo ya umeme; au
      (v) Cheti cha kufuzu cha Mtihani wa ujuzi wa umeme Daraja la II/ ngazi ya II au kinacholingana na hicho na miaka mitatu ya uzoefu katika masuala ya kazi za kufunga mifumo ya umeme.
      Daraja D Inatolewa ili kuweza kufanya kazi za ufungaji wa mifumo ya umeme katika msongo usiyozidi volti 230. Isipokuwa hataruhusiwa kufanya kazi yoyote iliyo chini ya leseni maalumu (S1, S2 na S3) pasipokuwa na leseni husika (i) Cheti cha kufuzu mtihanii wa ujuzi wa Umeme daraja la I, II, III, au Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi ngazi ya 4, Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi ngazi ya 5 au ainayolingana na hiyo katika ufundi wa ufungaji wa mifumo ya umeme; au

      (ii)mafunzo ya awali,kozi fupi, kozi za kati, cheti cha Juu cha Ufundi au cheti kinacholingana na hicho na uzoefu wa miaka mitatu katika kufunga mifumo ya umeme

      Daraja W Inatolewa ili kuweza kufanya kazi za ufungaji mifumo ya umeme chini ya usimamizi wa mwenye leseni Daraja A, B, S1, S2, S3, C au D. Mwombaji wa leseni anapaswa kuwa na mafunzo ya awali/kozi fupi/kozi ya kati, au cheti cha Juu cha ufungaji wa mifumo ya umeme au sifa nyinginezo kutoka Taasisi nyingine za Kiufundi zinazotambulika kutoa mafunzo ya ufungaji mifumo ya Umeme.
      Daraja S1 Inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme katika msongo wa aina zote. (i) Cheti cha Usajili cha Utaalam wa Uhandisi wa Umeme au /Umeme-Mitambo na miaka mitatu ya uzoefu wa kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme, mwaka mmoja kati ya hiyo iwe ni kufunga mifumo ya umeme katika msongo wa juu.
      (ii) Shahada ya Uhandisi wa Umeme au Uhandisi wa Umeme-Mitambo au
      Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 8 na miaka minne ya uzoefu wa kazi za ufungaji mifumo ya umeme ,miaka miwili kati ya hiyo iwe ni ufungaji wa mifumo ya umeme katika msongo wa juu wa umeme;
      (iii) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 7 au Stashahada ya Juu ya Uhandisi Umeme/ Umeme-Mitambo na miaka mitano ya uzoefu wa kazi katika masuala ya kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme, miaka mitatu kati ya hiyo iwe ya ufungaji mifumo ya msongo wa juu;
      (iv) Tuzo ya Kitaifa ya Ufundi Ngazi ya 6 au Cheti cha Ufundi sanifu katika masuala ya Uhandisi wa Umeme/Umeme-Mitambo na miaka sita ya uzoefu wa kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme, miaka minne kati ya hiyo iwe ya ufungaji umeme wa msongo wa juu
      Daraja S2 Inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme mpaka msongo wa volti 33,000 (i) Cheti cha Usajili cha Utaalamu Uhandisi wa Umeme/ Umeme-Mitambo na miaka mitatu ya uzoefu wa kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme, mwaka mmoja kati ya hiyo iwe ni kufunga mifumo ya umeme katika msongo wa kati; au
      (ii) Shahada ya Uhandisi wa umeme au Uhandisi wa Umeme- Mitambo au
      Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 8 na miaka mitatu ya uzoefu wa kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme, miaka miwili kati ya hiyo iwe ya ufungaji umeme katika msongo wa kati; au
      (iii) Tuzo ya Kitaifa ya Ufundi Ngazi ya 7 au zaidi, au Stashahada ya Juu ya Uhandisi Umeme/ Umeme-Mitambo na miaka minne ya uzoefu wa kazi katika masuala ya kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme, mwaka mmoja na nusu kati ya hiyo iwe ya ufungaji umeme katika msongo wa kati;
      Daraja S3 Inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme mpaka msongo wa volti 1,000 (i) Shahada ya Uhandisi wa Umeme/Umeme-Mitambo au Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 8 na zaidi au inayolingana na Shahada ya Uhandisi Umeme/Umeme-Mitambo na mwaka mmoja wa uzoefu wa kazi maalumu za kufunga mifumo ya umeme;
      (ii) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 7 au Stashahada ya Juu ya Uhandisi wa Umeme /Umeme-Mitambo au inayolingana na hiyo, na miaka miwili ya uzoefu wa kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme;
      (iii) Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 6 au Stashahada ya Kawaida ya Uhandisi Umeme/ Umeme-Mitambo au Cheti cha Ufundi kamili katika masuala ya uhandisi wa umeme au inayolingana na hiyo na miaka mitatu ya uzoefu wa kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme.
      (iv)Tuzo ya Kitaifa ya Kiufundi Ngazi ya 4 au Cheti cha kufuzu Mtihani wa Ujuzi wa Umeme Daraja la I, II au inayolingana na hiyo na miaka minne ya uzoefu wa kazi maalum za kufunga mifumo ya umeme.

      Na ifuatayo ni taarifa kuhusu gharama za leseni
      Aina/daraja la leseni Ada isiyorejeshwa (Shilingi) Ada ya nakala (kopi) ya leseni (Shilingi)
      A, B, S1, S2 130,000 20,000
      C, D, W, S3 50,000 20,000
      Muhimu: Ada isiyorejeshwa inalipwa mara moja kila baada ya miaka mitano, kwa kuwa muda wa kuhuisha leseni ni baada ya miaka mitano.

      Karibu.

        1. Ndugu Shabani,
          Tafadhali tazama kwenye barua pepe yako endapo EWURA imekutumia ujumbe kuhusu mustakabali wa leseni uliyoomba. Ikiwa hakuna ujumbe wowote kutoka kwetu, tupatie taarifa zako za maombi na namba ya simu kwa ufuatiliaji zaidi.

          Karibu

  21. Naomba kujuwa maendeleo ya leseni yangu ya umeme niliomba mwezi wa NNE(4) na je, ntaipata lini

  22. Mimi ni Fundi umeme lakini nimesomea course ya ELECTRONICS LEVEL-II katika department ya umeme,lakini na mimi nikihitaji leseni ya umeme yoyoye ile nitapata.Ninaomba msaada wenu hapa EWURA TZ

  23. Na pia mimi field yangu nilishawahi fanya TANESCO TEMEKE pale kurasini kwani napenda sana kazi yangu ya ufundi umeme.

  24. Habari naitwa emmanuel issaya msangi nipo pwani chalinze nimefanya maombi ya leseni ila mpka sasa sijapewa unaenda mwezi wa 3 sasa hivi . Msaada juu ya hilo

    1. Ndugu Emmanuel,
      Pole kwa kusubiri.
      Tafadhali tupatie namba yako ya simu na namba ya maombi ya leseni kwa ufuatiliaji.
      Asante

  25. JINA. HENRY KAMSIMOJA
    PHONE. 0625620684
    AIM. Naomba msaada nimelipia leseni ya umeme mpaka leo hakuna kinacho eleweka uhusu kupatiwa leseni

    1. Ndugu Hussein,
      Leseni hutolewa ndani ya siku 30 tangu kupokelewa na maombi kamili.Endapo kuna changamoto yoyote usisite kuwasiliana na EWURA
      Karibu

      1. Nilikuja kwenye ofisi za ewura ambazo zimehamishiwa mawasiliano lakini sijapata msaada maana mpaka sasa nikifungua kwenye akaunti yangu haifunguki nashindwa kuelewa labda mngenisaidia zaidi ili niweze kujua nafanyaje , je kama leseni imetoka nitajuaje maana toka nimelipia raehe 19oct22 .

    1. Ndugu Abdala,
      Tafadhali tembelea barua pepe yako endapo hujapata ujumbe kutoka EWURA tupigie 0800110030 (bure) muda na siku za kazi ili tuweze kufuatilia suala lako.

      Karibu

  26. habari mi naitwa anir nipo musoma nimejalibu kufungua acaunt ikakubali lakini nikijalibu kuingia ili nijisajili inagoma kufungunga naomba leseni ya umeme 0754476640

    1. Ndugu Abdallah,

      Tafadhali piga simu bila gharama kwenye namba 0800110030 ili kupata ushauri kuhusu suala lako. Simu hii hupatikana muda wa kazi tu saa 2asubuhi mpaka saa 10 kamili jioni, Jumatatu hadi Ijumaa.

  27. Mimi naitwa MAARUFU SALUM MASHUHURI NIME RENEW LESENI YANGU .CONTROL NAMBA NIMELIPIA 23/3/2023 ILA BADO SIJAIPATA MPAKA LEO TATIZO NINI

    1. Ndugu Maarufu,
      Endelea kuvuta subira, maombi yako yanafanyiwa kazi, yatakapokamilika utapata ujumbe kwenye simu na imeili yako. Na kwa sasa leseni zinatolewa kieletroniki hivyo utaweza kuchapisha leseni yako.

      Karibu

    1. Ndugu Maarufu,
      Endelea kuvuta subira, maombi yako yanafanyiwa kazi, yatakapokamilika utapata ujumbe kwenye simu na imeili yako. Na kwa sasa leseni zinatolewa kieletroniki hivyo utaweza kuchapisha leseni yako.

      Karibu

  28. Samahani Mimi nimesha jisajili kupitia LOIS na ikaniandikia “registration success” baada ya hapo sajaona muongozo wowote wa kuonesha naendea kupata leseni na elimu ya ufundi miaka miwili naomba kujua baada ya kujisajili na hii Lois nifanye nini sasa ili kukamilisha dhumuni maana nakosa Amani ya kutafta Riziki kupitia ujuzi nilio nao

  29. Habari za kazi hivi inachukua siku ngapi kupewa leseni Baada ya bodi kumaliza mchakato wa kukagua document zinazoomba leseni za umeme

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *