Ndugu William,
Mwombaji yeyote wa leseni ya rejareja ya mafuta, sharti afanye maombi kwa njia ya kieletroniki kupitia http://www.ewura.go.tz/lois. Taarifa muhimu zinazohitajika kuambatanishwa katika maombi hayo ni:
(a) Nakala ya nyaraka za usajili wa Kampuni au Leseni ya Biashara;
(b) Nakala ya Hati Miliki ya kiwanja palipojengwa kituo cha mafuta au uthibitisho
kutoka Mamlaka husika iliyoruhusu ujenzi wa kituo hicho.
(c) Nakala ya kibali cha ujenzi kutoka Halmashauri au Manispaa husika.
(d) Nakala ya Cheti cha Tathmini ya Athari ya Mazingira (Environmental Impact Assessment Certificate) kinachotolewa na Baraza la Hifadhi ya Mazingira.
(e) Nakala ya cheti cha mlipa kodi (TIN Certificate).
(f) Nakala ya cheti cha zima moto (Fire Safety Certificate) kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani.
(g) Kibali cha ujenzi kutoka EWURA (kwa vituo vilivyojengwa baada ya Aprili 2009).
(h) Orodha ya miundombinu iliyopo katika eneo hilo. Kwa upande wa matanki uooneshwe ujazo wake.
(i) Mchoro wa kituo ambao umesainiwa na Mhandisi aliyesajiliwa na Baraza la Wahandisi Tanzania ukionesha yafuatayo:
(i) umbali uliopo kati ya miundombinu ya kituo cha mafuta;
(ii) mahali pa kuingilia na kutokea kituoni;
(iii) mpaka wa kiwanja;
(iv) mahali pampu zinapotegemewa kufungwa; na
(j) Stakabadhi ya malipo ya ada ya maombi ya leseni.
MASHARTI YA KUPEWA LESENI YA REJAREJA YA KUENDESHA BIASHARA YA MAFUTA
Pamoja na kuwasilisha nyaraka zilizotajwa, kituo cha mafuta sharti kikaguliwe ili kuona kama kinakidhi masharti ya kupewa leseni. Masharti hayo ni pamoja na:
(a) Kuwa na vifaa vya kutosha vya kuzimia moto: Angalau ndoo moja ya mchanga na mtungi mmoja wa kilogramu 9 aina ya “ABE” kwa kila eneo ilipo pampu.
(b) Kuwepo switchi ya dharura iliyowekwa sehemu inayoonekana na kufikika kwa urahisi na mtu yeyote kwa ajili ya kuzima umeme. Swichi iandikwe “SWICHI YA DHARURA”.
(c) Kuwepo na vyoo safi na vya kutosha kwa ajili ya wafanyakazi wa kituo na wateja kwa ujumla. Viwepo vyoo vya wanaume na wanawake.
(d) Alama za kutosha za usalama zinazoonekana vizuri na mteja anapoingia hapo kituoni. Alama hizo ni pamoja na: Zima Injini, Zima Simu na Usivute Sigara.
(e) Matanki, vifaa vya kupimia ujazo wa matanki (dip rods) na pampu lazima viwe vimehakikiwa na Wakala wa Vipimo (WMA). Aidha, pampu sharti ziwe katika hali nzuri ya kufanya kazi.
(f) Mifuniko ya sehemu ya kushushia mafuta na pampu sharti iandikwe ili kuonesha aina ya mafuta yaliyomo au yanayouzwa.
(g) Mifuniko ya matanki ya mafuta sharti ipakwe rangi zifuatazo: Petroli – Nyekundu, Dizeli – Njano na Mafuta ya taa – Bluu
(h) Kila mfuniko wa tanki na mahali pa kuteremshia mafuta vitengenezwe kulingana na viwango vinavyokubalika katika tasnia ya mafuta.
(i) Kituo kiwe kimesakafiwa kwa zege angalau mita nne (4) kuzunguka maeneo yote ya pampu na mahali pa kushushia mafuta na pia kiwe na mfereji uliojengwa vizuri na unaoungana na kitenganisha maji na mafuta (oil/water separator).
(j) Kitenganisha maji na mafuta sharti kiwe na vyumba (chemba) vitatu na kila chumba kiwe na urefu usiopungua mita 1, upana wa mita 2 na kimo cha mita 1. Pia, sharti kiwe na mfuniko unaoweza kufunguliwa kwa urahisi na kuwekwa vali ya kufunga na kufungua mahali pa kutolea maji safi.
(k) Kila tanki la mafuta liwe limeunganishwa na bomba la kupumulia (vent pipe) lenye kimo kisichopungua mita 3.5. Bomba hizo ziwe angalau mita 1.5 kutoka jengo lolote na angalau mita 4.5 kutoka chanzo chochote cha kuingiza hewa au kusababisha moto kama vile dirisha, kiyoyozi, jenereta n.k.
(l) Eneo la pampu liwe limejengewa vizuizi vya kukinga pampu zisigongwe na gari (crush barriers). Vizuizi hivyo viwe na kimo kisichopungua mita moja kutoka sakafu ya kituo.
(m) Kituo kiwe kimejengewa paa (canopy) linalokidhi viwango vinavyotakiwa katika ujenzi wa vituo vya mafuta. Kimo cha paa kisipungue mita 5 na upana wa mita 3 kila upande kutoka katikati ya pampu.
(n) Kituo kiwe katika hali ya usafi.
(o) Kuwepo kwa waya wa kuzuia mwako wa umeme (spark) ambao unaunganishwa na gari la mafuta wakati wa kuteremsha mafuta.
Kituo cha mafuta kinachokidhi masharti tajwa hapo juu, ndicho hupewa leseni na EWURA. Vituo vya mafuta ambavyo havikidhi masharti ya kupewa leseni, haviruhusiwi kufanya biashara hadi hapo vitakapokuwa vimekidhi masharti yote.
ADA NA MUDA WA UHAI WA LESENI
Ada ya leseni ni Shillingi milioni moja (1.000.000/=). Muda wa leseni ni miaka mitano (5). Baada ya uhai wa leseni, mwenye kituo anatakiwa aombe kuhuisha leseni kwa kujaza fomu ya maombi na kuileta EWURA.
Ndugu Michael,
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako. Endapo utakuwa na swali au kuhitaji ufafanuzi zaidi, piga simu BURE 0800110030 au andika barua pepe info@ewura.go.tz.
Vilevile unaweza kufika katika Ofisi zetu za makao makuu Dodoma au Kanda zilizopo Arusha, Dar es Salaam, Mbeya,Mwanza na Kanda ya Kati Dodoma.
Karibu.
MADARAJA YA LESENI ZA UMEME YANAYOTOLEWA NA EWURA
Leseni Daraja A: inatolewa ili kufanya kazi za umeme katika msongo wa aina zote isipokuwa kazi zilizoruhusiwa chini ya daraja “S1, S2 na S3”.
Leseni Daraja B: inatolewa ili kufanya kazi za umeme mpaka msongo wa kati (33,000V) isipokuwa kazi zilizoruhusiwa chini ya daraja “S1, S2 na S3”.
Leseni Daraja C: inatolewa ili kufanya kazi za umeme mpaka msongo wa chini (400V) isipokuwa kazi zilizoruhusiwa chini ya daraja “S1, S2 na S3”.
Leseni Daraja D: inatolewa ili kufanya kazi za umeme katika msongo wa njia moja (230V) isipokuwa kazi zilizoruhusiwa chini ya daraja “S1, S2 na S3”.
Leseni Daraja W: inatolewa ili kuweza kufanya kazi za ufungaji mifumo ya umeme chini ya usimamizi wa mwenye leseni Daraja A, B, C au D.
Leseni Daraja “S1”: inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme katika msongo wa umeme wa aina zote.
Leseni Daraja “S2”: inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme mpaka msongo wa volti 33,000; na
Leseni Daraja “S3”: inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme mpaka msongo wa volti 1,000.
Ndugu Samson,
Tafadhali pitia maelezo yafuatayo kwa ufafanuzi zaidi:-
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
1. Utangulizi
1.1 Mahitaji ya mafuta ya petroli na dizeli maeneo ya vijijini yanazidi kuongezeka. Ongezeko hili linatokana na kushamiri kwa shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na usafiri wa pikipiki maarufu kama “boda boda”.
1.2 Hata hivyo, maeneo mengi ya vijijini hayana vituo vya mafuta kutokana na ukweli kwamba, wawekezaji wa biashara hiyo wenye mitaji mikubwa husita kujenga vituo vya kuuzia mafuta Vijijini kwa kuona maeneo hayo hakuna biashara ya kutosha .
1.3 Matokeo yake, wafanyabiashara wenye mitaji midogo na wasio na uzoefu katika biashara ya mafuta, huingia kwenye biashara hii. Kutokana na mitaji yao midogo na kutokuwa na uzoefu, wafanyabiashara hawa huanza kufanya biashara ya mafuta kwa kutumia miundo mbinu hafifu na isiyo salama kama vile kuhifadhi mafuta kwenye mapipa, madumu ya plastiki na kuyauza kwa kutumia chupa za plastiki au njia nyingine isiyo salama.
1.4 Uhifadhi wa mafuta kwa namna hiyo ni hatari kwa Usalama, Afya na Mazingira. Ni dhahiri kuna matukio mengi ya moto ambayo yamesababishwa na uhifadhi wa mafuta majumbani au kwenye vibanda vya biashara. Ajali hizo za moto, zimegharimu maisha ya watu na kuharibu mali. Pia, wafanyabishara katika maeneo hayo wako hatarini kupata magonjwa ya kansa ya ngozi kutokana na kushika mafuta wakati wa kutoa huduma hiyo. Kwa upande mwingine, mafuta humwagika ardhini na kuharibu mazingira.
1.5 Kuhifadhi mafuta kutumia vyombo vya plastiki kunaharibu ubora wa mafuta hayo na hasa mafuta ya petroli. Mafuta na vyombo vya plastiki vina asili moja. Ubora wa mafuta ya petroli pia unaweza kuathiriwa na mwanga wa jua. Hivyo, vyombo vya moto vinavyo tumia mafuta yanayohifadhiwa kwenye vyombo vya plastiki viko hatarini kupata madhara kwa sababu ya kutumia mafuta ambayo hayana ubora unaohitajika.
1.6 Biashara ya mafuta ya petroli ni muhimu sana, lakini ni hatari ikiwa itafanyika kiholela bila kufuata misingi ya usalama na viwango. Hivyo ni vyema mafuta ya petroli yakahifadhiwa na kuuzwa kwenye miundombinu ambayo imetengenezwa kwa ajili ya kazi hiyo. Lengo ni kulinda usalama, afya, ubora wa mafuta na mazingira.
1.7 Moja ya miundombinu ambayo inatimiza lengo tajwa hapo juu ni vituo vya kuuzia mafuta. Sababu kubwa ni kuwa, kwenye kituo cha mafuta, matenki ya kuhifadhia mafuta yanafukiwa chini ya ardhi. Hivyo, hata moto ukitokea si rahisi mafuta yaliyo ndani ya matenki hayo kulipuka.
1.8 Kipeperushi hiki kimelenga kutoa maelezo kwa kifupi juu ya ujenzi wa vituo vya gharama nafuu kwa kuelezea vitu muhimu na vya msingi vinavyotakiwa kuzingatiwa wakati wa kujenga kituo cha mafuta. Vilevile, Kipeperushi hiki kinaelezea Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini ambazo zilitungwa mahsusi kwa ajili ya kupunguza gharama za uwekezaji wa vituo hivyo.
1.9 Ni lengo la EWURA kutengeneza mazingira ambapo watu wa Vijijini wanakuwa na haki sawa na watu wa Mijini katika upatikanaji wa bidhaa ya mafuta kwa hali ya ubora na usalama unaohitajika na kwa bei nafuu.
1.10 Ni matumaini ya EWURA kwamba, Kipeperushi hiki kitatoa mwanga kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa mafuta ya petroli nchini namna ambavyo uwekezaji wa vituo vya mafuta Vijijini unavyoweza kufanywa kwa gharama nafuu na kuwawezesha watumiaji wa mafuta hayo kupata huduma nzuri zaidi na salama bila kumuathiri mfanyabiashara wa mafuta.
2 Mahitaji na Mambo ya Kuzingatia Wakati wa Ujenzi
Ili uweze kujenga kituo unatakiwa kuzingatia yafutatayo:
(a) Uwe na kiwanja ambacho Mamlaka husika (mfano: Halmashauri ya kijiji) imeridhia kitumike kwa ajili ya biashara ya kituo cha mafuta. Ili kukidhi viwango vya usalama (safety distance requirements), kiwanja kinachofaa kujenga kituo cha mafuta kinatakiwa angalau kiwe na ukubwa wa mita za mraba 400.
(b) Uwe angalau na tenki moja (1) la kuhifadhia mafuta. Kama utauza aina zaidi ya moja ya mafuta, matenki yaongezeke sawia. Tenki liwe na ujazo wa angalau lita 4,500 au 5,000.
Uwe na pampu yenye mkono mmoja au miwili kulingana na aina za mafuta.
(c) Bomba nne (4) za chuma za inchi nne (inchi ) na urefu wa mita tano (mita 5) kwa ajili ya kujengea paa (canopy). Pia, utahitaji bomba za inchi moja au inchi 1.5 na bati kwa ajili ya kenchi na kuezeka (angalia Mchoro Na 2). Bomba za kenchi zinatakiwa kuwa na urefu wa mita saba (mita 7).
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia wakati wa ujenzi:
(a) Matenki ya kuhifadhia mafuta inabidi yafukiwe ardhini kwa umakini mkubwa. . Kwa sehemu ambazo maji ya ardhini (water table) yapo karibu, ni vizuri matenki yakajengewa zege.
(b) Matenki yapakwe rangi ya kuzuia kutu. Pia, matenki yanatakiwa yafukiwe na mchanga kwa ajili ya kuzuia kutu.
(c) Kituo kinatakiwa kisakafiwe kwa zege imara la angalau inchi nne (inchi 4). Eneo mahsusi la kusakafia ni eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta (angalia Mchoro Na 1). Eneo linalozunguka pampu liwe na ukubwa wa angalu mita za mraba 45 (yaani upana mita 6.4 na urefu mita 7). Eneo la kushushia mafuta linatakiwa liwe na ukubwa wa angalau mita za mraba 16 (yaani upana mita 4 na urefu mita 4) ili gari la mafuta liweze kusimama kwenye zege hiyo wakati wa kushusha mafuta.
(d) Eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta ijengewe mitaro inayoelekea kwenda kwenye chemba ya kuchuja mafuta na maji (Oil/water separator). Chemba ya kuchuja mafuta na maji inatakiwa iwe na vyumba vitatu. Kila chumba kiwe na urefu wa mita moja (mita 1), upana mita mbili (mita 2) na kina mita moja (mita 1). Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo. Usitumie zege, ili iwe rahisi wakati wa kusafisha (angalia Mchoro Na 3).
(e) Kituo kinatakiwa kiwe na paa imara (canopy) kama inavyoonyesha kwenye Mchoro Na 2. Paa linatakiwa kuwa na urefu wa mita 5.
(f) Ni vyema kutumia wahandisi wa ujenzi au mafundi wenye uzoefu wa ujenzi wa vituo vya mafuta.
3 Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini
EWURA imeandaa Kanuni mahsusi kwa ajili ya ujenzi na biashara ya vituo vya mafuta vijijini. Kwa mujibu wa kanuni hizo, mtu yeyote anayetaka kujenga kituo kijijini ni lazima kabla ya kuanza ujenzi apate kibali cha EWURA, baada ya kutuma maombi ya kupewa kibali hicho. Pia, kabla ya kuanza biashara, mwekezaji anatakiwa kuwa na leseni ya EWURA, ambayo hutolewa baada ya EWURA kupokea maombi yaliyozingatia mahitaji yote. Baada ya hapo, EWURA itakagua kituo husika ili kujiridhisha kuwa kinakidhi viwango.
Mchoro Na 1: Ramani ya Kituo cha mafuta inayoonyesha tenki, pampu, ofisi, barabara ya kuingia na kutoka kituoni.
Mchoro Na 2: Picha ikionyesha paa la kituo (canopy).
.
Mchoro Na 2: Chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator)
Mchoro Na 3: Picha namna chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator) inavyotakiwa kujengwa. Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo.
Almost makadilio kama tsh ngap kinaweza kukamilika kituo hicho
Ndugu Simon,
Kituo cha mafuta maeneo ya vijijini vinakadiriwa kugharimu kati ya milioni 50-70. Hata hivyo gharama inaweza kubadilika kutokana na masuala mbalimnali ikiwemo gharama za malighafi. Vituo vya mijini gharama yake inategemea na ukubwa wa kituo
Karibu
Kufungua kituo wilayani au mijini inabidi kuwepo na utofauti wa kilomiter ngap au mita ngapi baina ya kituo nakituo?
Bwana Tito,
Ada ya maombi ni tsh 10,000/ na malipo ya leseni inategemea na daraja lako la leseni, kiwango cha juu kabisa ni tsh 120,000/ kwa daraja A. Na inaendelea kushuka mpaka kufikia wiremen. Nakushauri upitie Kanuni za Ufungaji meme za mwaka 2019, zilizopo katika tovuti yetu, ukurusa wa Umeme.
Kwa maelezo zaidi piga simu bure 0800110030
Karibu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Nawapongeza kwa Kazi bora mnayoifanya kwa muujibu wa
Maelezo yenu mtandaoni.
Habari
Mara nyingi tunajua bei ya petrol inavouzwa ila inakonunuliwa napataje kujua bei zake kwa kila msimu je natumia website gan kujua au link ipi au nifanyaje nipate kujua bei ya manunuzi
Ndugu Joseph, ununuzi wa mafuta yanayotumika nchini hufanywa kwa pamoja kwa uratibu wa Wakala ya Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) na mafuta hununuliwa katika soko la dunia. Pitia https://www.pbpa.go.tz/ ili uweze kupata taarifa zaidi.
Karibu
Bwana Lugoe,
Ada ya leseni ni Shillingi milioni moja (1.000.000/=). Na muda wa leseni ni miaka mitano (5).
Kumbuka:- Maombi ya leseni hufanyika kwa njia ya mtandao kupitia kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Kwa maelezo zaidi piga 0800110030.
Karibu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Ndugu Focus, utaratibu umetumwa katika barua pepe yako.
Karibu
Naomba pia utalatibu wa kufungua kituo cha mafuta.
Ndugu Edgar,
Tafadhali rejea barua pepe yako.
Karibu
Nimepata taarifa kuwa Ewura mmerahisisha taratibu za kujenga kituo cha mafuta kijijini kwa gharama nafuu tofauti na mjini. Naomba kujua vi vitu gani vya kuzingatia ili niweze kuwekeza kituo cha mafuta vijijini.
Habari Sammy,
Nakutumia kipeperushi kwa email ukipitie. Endapo utakuwa na swali lolote usisite kuwasiliana nasi. Pia unaweza kupiga simu bure kwa namba 0800110030
Nahitaji kujua taratibu za kufungua kituo Cha mafuta yaan Petro station kijijin
Email yangu ni henryjane49@gmail.com
Tafadhali naomba kujua taratibu zake
Nami naitaji mnipe mwongozo mzuma wa kufungua kituo kidogo cha mafuta ikiwa ni petrol tuu
Ndugu Gerald,
Mwongozo huo ufuatao:-
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
1. Utangulizi
1.1 Mahitaji ya mafuta ya petroli na dizeli maeneo ya vijijini yanazidi kuongezeka. Ongezeko hili linatokana na kushamiri kwa shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na usafiri wa pikipiki maarufu kama “boda boda”.
1.2 Hata hivyo, maeneo mengi ya vijijini hayana vituo vya mafuta kutokana na ukweli kwamba, wawekezaji wa biashara hiyo wenye mitaji mikubwa husita kujenga vituo vya kuuzia mafuta Vijijini kwa kuona maeneo hayo hakuna biashara ya kutosha .
1.3 Matokeo yake, wafanyabiashara wenye mitaji midogo na wasio na uzoefu katika biashara ya mafuta, huingia kwenye biashara hii. Kutokana na mitaji yao midogo na kutokuwa na uzoefu, wafanyabiashara hawa huanza kufanya biashara ya mafuta kwa kutumia miundo mbinu hafifu na isiyo salama kama vile kuhifadhi mafuta kwenye mapipa, madumu ya plastiki na kuyauza kwa kutumia chupa za plastiki au njia nyingine isiyo salama.
1.4 Uhifadhi wa mafuta kwa namna hiyo ni hatari kwa Usalama, Afya na Mazingira. Ni dhahiri kuna matukio mengi ya moto ambayo yamesababishwa na uhifadhi wa mafuta majumbani au kwenye vibanda vya biashara. Ajali hizo za moto, zimegharimu maisha ya watu na kuharibu mali. Pia, wafanyabishara katika maeneo hayo wako hatarini kupata magonjwa ya kansa ya ngozi kutokana na kushika mafuta wakati wa kutoa huduma hiyo. Kwa upande mwingine, mafuta humwagika ardhini na kuharibu mazingira.
1.5 Kuhifadhi mafuta kutumia vyombo vya plastiki kunaharibu ubora wa mafuta hayo na hasa mafuta ya petroli. Mafuta na vyombo vya plastiki vina asili moja. Ubora wa mafuta ya petroli pia unaweza kuathiriwa na mwanga wa jua. Hivyo, vyombo vya moto vinavyo tumia mafuta yanayohifadhiwa kwenye vyombo vya plastiki viko hatarini kupata madhara kwa sababu ya kutumia mafuta ambayo hayana ubora unaohitajika.
1.6 Biashara ya mafuta ya petroli ni muhimu sana, lakini ni hatari ikiwa itafanyika kiholela bila kufuata misingi ya usalama na viwango. Hivyo ni vyema mafuta ya petroli yakahifadhiwa na kuuzwa kwenye miundombinu ambayo imetengenezwa kwa ajili ya kazi hiyo. Lengo ni kulinda usalama, afya, ubora wa mafuta na mazingira.
1.7 Moja ya miundombinu ambayo inatimiza lengo tajwa hapo juu ni vituo vya kuuzia mafuta. Sababu kubwa ni kuwa, kwenye kituo cha mafuta, matenki ya kuhifadhia mafuta yanafukiwa chini ya ardhi. Hivyo, hata moto ukitokea si rahisi mafuta yaliyo ndani ya matenki hayo kulipuka.
1.8 Kipeperushi hiki kimelenga kutoa maelezo kwa kifupi juu ya ujenzi wa vituo vya gharama nafuu kwa kuelezea vitu muhimu na vya msingi vinavyotakiwa kuzingatiwa wakati wa kujenga kituo cha mafuta. Vilevile, Kipeperushi hiki kinaelezea Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini ambazo zilitungwa mahsusi kwa ajili ya kupunguza gharama za uwekezaji wa vituo hivyo.
1.9 Ni lengo la EWURA kutengeneza mazingira ambapo watu wa Vijijini wanakuwa na haki sawa na watu wa Mijini katika upatikanaji wa bidhaa ya mafuta kwa hali ya ubora na usalama unaohitajika na kwa bei nafuu.
1.10 Ni matumaini ya EWURA kwamba, Kipeperushi hiki kitatoa mwanga kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa mafuta ya petroli nchini namna ambavyo uwekezaji wa vituo vya mafuta Vijijini unavyoweza kufanywa kwa gharama nafuu na kuwawezesha watumiaji wa mafuta hayo kupata huduma nzuri zaidi na salama bila kumuathiri mfanyabiashara wa mafuta.
2 Mahitaji na Mambo ya Kuzingatia Wakati wa Ujenzi
Ili uweze kujenga kituo unatakiwa kuzingatia yafutatayo:
(a) Uwe na kiwanja ambacho Mamlaka husika (mfano: Halmashauri ya kijiji) imeridhia kitumike kwa ajili ya biashara ya kituo cha mafuta. Ili kukidhi viwango vya usalama (safety distance requirements), kiwanja kinachofaa kujenga kituo cha mafuta kinatakiwa angalau kiwe na ukubwa wa mita za mraba 400.
(b) Uwe angalau na tenki moja (1) la kuhifadhia mafuta. Kama utauza aina zaidi ya moja ya mafuta, matenki yaongezeke sawia. Tenki liwe na ujazo wa angalau lita 4,500 au 5,000.
Uwe na pampu yenye mkono mmoja au miwili kulingana na aina za mafuta.
(c) Bomba nne (4) za chuma za inchi nne (inchi ) na urefu wa mita tano (mita 5) kwa ajili ya kujengea paa (canopy). Pia, utahitaji bomba za inchi moja au inchi 1.5 na bati kwa ajili ya kenchi na kuezeka (angalia Mchoro Na 2). Bomba za kenchi zinatakiwa kuwa na urefu wa mita saba (mita 7).
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia wakati wa ujenzi:
(a) Matenki ya kuhifadhia mafuta inabidi yafukiwe ardhini kwa umakini mkubwa. . Kwa sehemu ambazo maji ya ardhini (water table) yapo karibu, ni vizuri matenki yakajengewa zege.
(b) Matenki yapakwe rangi ya kuzuia kutu. Pia, matenki yanatakiwa yafukiwe na mchanga kwa ajili ya kuzuia kutu.
(c) Kituo kinatakiwa kisakafiwe kwa zege imara la angalau inchi nne (inchi 4). Eneo mahsusi la kusakafia ni eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta (angalia Mchoro Na 1). Eneo linalozunguka pampu liwe na ukubwa wa angalu mita za mraba 45 (yaani upana mita 6.4 na urefu mita 7). Eneo la kushushia mafuta linatakiwa liwe na ukubwa wa angalau mita za mraba 16 (yaani upana mita 4 na urefu mita 4) ili gari la mafuta liweze kusimama kwenye zege hiyo wakati wa kushusha mafuta.
(d) Eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta ijengewe mitaro inayoelekea kwenda kwenye chemba ya kuchuja mafuta na maji (Oil/water separator). Chemba ya kuchuja mafuta na maji inatakiwa iwe na vyumba vitatu. Kila chumba kiwe na urefu wa mita moja (mita 1), upana mita mbili (mita 2) na kina mita moja (mita 1). Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo. Usitumie zege, ili iwe rahisi wakati wa kusafisha (angalia Mchoro Na 3).
(e) Kituo kinatakiwa kiwe na paa imara (canopy) kama inavyoonyesha kwenye Mchoro Na 2. Paa linatakiwa kuwa na urefu wa mita 5.
(f) Ni vyema kutumia wahandisi wa ujenzi au mafundi wenye uzoefu wa ujenzi wa vituo vya mafuta.
3 Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini
EWURA imeandaa Kanuni mahsusi kwa ajili ya ujenzi na biashara ya vituo vya mafuta vijijini. Kwa mujibu wa kanuni hizo, mtu yeyote anayetaka kujenga kituo kijijini ni lazima kabla ya kuanza ujenzi apate kibali cha EWURA, baada ya kutuma maombi ya kupewa kibali hicho. Pia, kabla ya kuanza biashara, mwekezaji anatakiwa kuwa na leseni ya EWURA, ambayo hutolewa baada ya EWURA kupokea maombi yaliyozingatia mahitaji yote. Baada ya hapo, EWURA itakagua kituo husika ili kujiridhisha kuwa kinakidhi viwango.
Mchoro Na 1: Ramani ya Kituo cha mafuta inayoonyesha tenki, pampu, ofisi, barabara ya kuingia na kutoka kituoni.
Mchoro Na 2: Picha ikionyesha paa la kituo (canopy).
.
Mchoro Na 2: Chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator)
Mchoro Na 3: Picha namna chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator) inavyotakiwa kujengwa. Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo.
Bwana Sammy karibu.
Ni kweli. Tafadhali tupatie anuani ya barua pepe ili upate kipeperushi chenye maelezo husika.
Karibu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Naomba kujua taratibu za kufungua KITUO kidogo cha kuuza mafuta.
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako. Karibu
Ndugu Gerald,
Gharama ya maombi ya leseni ni shilingi 10,000/
Ada ya leseni inatofautiana kwa aina ya leseni kuanzia shilingi 40,000 mpaka 150,000/
Ada zote hudumu kwa muda wa miaka mitatu.
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Bwana Kijika,
Leseni hutolewa ndani ya siku 30 za kazi baada ya kupokea maombi kamili. Endapo una suala au changamoto yoyote wasiliana nasi na unaweza kupiga simu bure 0800110030.
Karibu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Habari, ningependa kujua utaratibu na documents zinazotumika kuomba kibali au leseni ya kufanya biashara ya kuuza vilainishi/ lubricants kwa kampuni. Kama kuna kipeperushi tafadhali naomba nisaidiwe.
Asante
Ndugu Makota,
Utaratibu unaotumika ni kufanya maombi kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa kieletroniki kwa kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/.
Pia pitia ukurasa huu https://www.ewura.go.tz/approval-and-licencing/ kwa maelezo zaidi.
Pia tutumie email yako tafadhali.
Na unaweza kupiga simu 0800110030 (bure) kwa maelezo zaidi au ufafanuzi.
Karibu
Naomba kujua garama za kuanzisha kituo kidogo cha mafuta nalenga boda boda na baadhi ya magari kwa upande wa vijijini.maana nimesikia kuna gharama kidogo nafuu.
Ndugu Kafyome,
Tfadhali,makadirio ya gharama ni takribani milioni 55. Hata hivyo gahrama hii inaweza kuzidi kidogo au kupungua kwa sababu mbalimbali.
Naomba utume anuani yako ya barua pepe ili tukutumie maelezo husika.
Asante
Maombi hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu na kubofya LOIS, kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Tafadhali naomba kupata makadirio ya uanzishaji wa kituo kidogo cha mafuta kijijini na utaratibu wake. Nalenga watu wa bodaboda na magari pia mashine za kusaga.
Email yangu ni jsumni@gmail.com
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki— https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Karibu
Hellow ewura ,
Good job,ina eneo langu njia ya kuelekea msumi mbezi DSM ina mapango wa kujenga kituo cha mafuta.naomba kufahamishwa taratibu za kuanza kujenga Hadi nafungua kituo .thanks
Good job
Habari za Asubuhi
Hongereni kwa kazi kubwa mnayofanya
Naomba kuuliza: Nina mpango kwa kuanzisha Kituo Kidogo cha Mafuta au pump kwa ajili ya kuhudumia watu wa Kijijini kwani Sheli zipo mbali. Naomba kupata utaratibu ili niweze kujua kama nitaweza.
Habari, Ewura kulikuwa na mpango wa kuanza kutoa vibali kwa ajili ya uanzishwaji wa mobile petrol station (Guta Petrol Station) haswa kwa maeneo ya vijijini. Tafadhali naweza kupata maelezo zaidi juu ya utolewaji wa leseni ya vituo hivyo vya mafuta na taratibu za kufuatwa. Na je Fuel dispenser ya aina yoyote inaweza kutumika katika uuzaji wa mafuta au kuna aina za dispenser ndio zinazokidhi vigezo?. Na naomba kupata kipeperushi cha uanzishaji wa kituo cha mafuta vijijini.
email masaganya07@hotmail.com
Ndugu George,
Utaratibu wa vituo tembezi (mobile petrol stations) bado haujakamilika. Utakapokuwa tayari au vinginevyo taarifa itatolewa. Kuhusu kipeperushi,tafadhali rejea ktk barua pepe yako.
Kwa maelezo zaidi piga 080011030 BURE
Asante
Niko interested na kupata maelezo ya kuwa na hizi mobile fuel station, na pia hiyo namba ambayo ni ya huduma kwa mteja haipatikani. tunaomba msaada zaidi
Pia namimi naomba kupata nakala ya maelezo ya hizo petrol station ndogo vijijini.
Ndugu Mohamed,
Ukubwa wa eneo inategemea aina ya kituo na mahali kinapojengwa. Kwa maeneo ya vijini ni kuanzia mita za mraba 400.
Kwa maelezo zaidi tupigie 0800110030 bila gaharama.
Karibu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Kipeperushi kimetumwa katika barua pepe yako. Karibu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Ndugu Jane,
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako. Utaratibu huu unatumika ni kwa maeneo yote. Tofauti ni katika aina ya kituo na eneo linalohtajika. Kwa maeneo ya Dar es Salaam, ukubwa wa eneo ni kuanzia sq 1500 mpaka 2400.
Aidha, Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Karibu.
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako
Habari Ewura, niko kwenye utafiti wa gharama za kujenga kituo cha mafuta mjini , gharama zisiuhusishe eneo. Nimejaribu kutafuta mwenyewe nimepata majibu mchanganyiko. Naomba msaada tafadhari.
Ndugu James,
Hongera kwa kazi hiyo.
Tunashauri utupatie majibu mchanganyiko uliyopata ili tuweze kubaini endapo umepata majibu sahihi ama la.
Hata hivyo, Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Naomba kipeperushi chenye utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta vijijini. Niliomba hapo kabla kwenye uzi wa mtu mwingine. Pia kama utaratibu wa kuuza kwa kutumia guta/kirikuu kama umekamilika tafadhali ambatanisha vipeperushi vyote. Asante
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Utaratibu wa vituo tembezi bado haujakamilika. Karibu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako. Karibu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako. Karibu
Habari za leo Muheshimiwa, Eweru ningependa kupata information zozote kuhusu kufungua kituo cha mafuta mjini na kijijini pia. Ikiwa nchini au nchini jirani hususani nchi toka Maziwa Makuu. Na nijinsi gani pia mnaweza kusaidia kufanikisha swala la ufunguaji kituo cha mafuta.
Maombi hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu na kubofya LOIS, kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Mimi nipo nyumba ya mungu, Simanjiro, naomba muongozo wa hatua ninazopaswa kufuata ninapotaka kufungua kituo cha mafuta, napenda kujua procedures na gharama za ada za serikali. Tayari nimeshachimba visima vya kuweka matanki
Habari.
Tafadhali naomba kupatiwa utaratibu wa kupata lesini ya uuzaji wa mafuta ya petroli na dizeli kwa njia ya mobile (yaani kuuza mafuta bila kua na kituo cha mafuta yaani kwa kutumia gari yenye tenki na pampu)
Habari,
Nimeomba Construction approval kwa ajili ya kituo caha mafuta , nimefuatilia hatua na kuona ipo hatua ya Review and Approval , je baada ya hatua io kuna hatua zaidi , na kama zipo bado ngapi hadi kuweza kupata kibari cha ujenzi !
Asante
Sanga .
Napenda kujua taratibu /muongozo kamili wa Kuanzisha kituo cha mafuta kiwe kidogo,cha kati au kikubwa mjini au kijijini,ili kuona ni wapi naweza jikita.
Habari team EWURA.
Mimi ni mdau wa sekta ya mafuta.Napenda kufahamu sasa muongozo kamili na gharama za kuanzisha kituo cha mafuta kwa mjini na ama kijijini kiwe kikubwa au kidogo.
Nitashkuru ombo langu likifanyiwa kazi na kupata majibu
Habari, ninaitwa Nelson tafadhali naomba kujua taratibu za kufuata pamoja na ada husika ili kuweza kupata kibali cha kuuza mafuta (yaani petroli na dizeli) kwa njia ya mobile (kwa kutumia gari zenye tanki zilizofungwa pampu). Asante.
Habari,
Nahitaji kuwa mfanya biashara wa mafuta (liquid)vijijini je naweza kupata mwangaza wa pa kuanzia,na naomba kupata vipeperushi vinavyotoa miongozo email yangu ni hakimusadock@gmail.com
Nathamini na kuheshimu kazi nzuri ambazo EWURA imekuwa ikifanya kwa maendeleo ya Taiga letu. Naomba nisaidiwe kipeperushi cha kufahamu namna ya uanzishaji na ufunguaji wa kituo cha mafuta vijijini.
Ndugu Alson, vituo vya mafuta kuuziana mafuta haina tatizo kwa sababu ni maelewano yao. Jambo la msingi ni kuhakikisha katika kufanya hivyo hawavunji sheria. Hata hivyo ni kwa mujibu wa Kifungu cha 26(2)(b)(ii) cha Kanuni za Bidhaa za Mafuta (Jumla, Rejareja, Kuhifadhi na Matumizi Binafsi),Tangazo la Serikali Na . 817 la mwaka 2020, kila mmoja anapaswa kuingia mkataba wa mauziano ya mafuta na wauzaji wa mafuta kwa ujumla.
Karibu
Habari za leo, naomba kupewa utaratibu wa kuanzisha na kusajili kituo cha uuzaji mafuta (petrol na diesel) kijijini. Ingekuwa vyema nikaelekezwa hatua ya kwanza mpaka ya mwisho ikiwa tayari nina eneo ambalo ndilo natarajia kulitumia kwa shughuli/biashara hiyo. Pamoja na uwanja huu ni vyema nipewe majibu kwa barua pepe yangu. Asante
Hello
Nahitaji kuanzisha kituo Kidogo cha mafuta (Mini Petrol Station) Kigoma vijijini. Nisaidieni hatua za kufuata, sample bajeti structure, kusajili na kupata leseni
Ndugu Michael,
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako, hata hivyo, maeneo ya vijijini na mijini ni ukubwa wa eneo ambao kwa mjini ni mita za mraba 1200 hadi 2400 kulingana na aina ya kituo kinachokusudiwa kujengwa.
Endapo utahitaji taarifa zaidi usisiste kuwasiliana nasi.
Karibu
Ndugu Jacquiline,
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako, hata hivyo, maeneo ya vijijini na mijini ni ukubwa wa eneo ambao kwa mjini ni mita za mraba 1200 hadi 2400 kulingana na aina ya kituo kinachokusudiwa kujengwa.
Endapo utahitaji taarifa zaidi usisiste kuwasiliana nasi.
Karibu
Habari, naomba kufahamu kuna maeneo yanahesabika yapo mjini lakini kiuhalisia ni kijijini kabisa. Kwa mfano kayenze mwanza. Inahesabika iko ndani ya manispaa ya ilemela lakini kwa waopajua ni kijijini kabisa. Hapo inakaaje kuhusu lile swala la leseni zenu za kurahisisha huduma kwa wanakijiji kama hao? Masharti yatabaki yale yale kama ya kituo cha mjini?
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
1. Utangulizi
1.1 Mahitaji ya mafuta ya petroli na dizeli maeneo ya vijijini yanazidi kuongezeka. Ongezeko hili linatokana na kushamiri kwa shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na usafiri wa pikipiki maarufu kama “boda boda”.
1.2 Hata hivyo, maeneo mengi ya vijijini hayana vituo vya mafuta kutokana na ukweli kwamba, wawekezaji wa biashara hiyo wenye mitaji mikubwa husita kujenga vituo vya kuuzia mafuta Vijijini kwa kuona maeneo hayo hakuna biashara ya kutosha .
1.3 Matokeo yake, wafanyabiashara wenye mitaji midogo na wasio na uzoefu katika biashara ya mafuta, huingia kwenye biashara hii. Kutokana na mitaji yao midogo na kutokuwa na uzoefu, wafanyabiashara hawa huanza kufanya biashara ya mafuta kwa kutumia miundo mbinu hafifu na isiyo salama kama vile kuhifadhi mafuta kwenye mapipa, madumu ya plastiki na kuyauza kwa kutumia chupa za plastiki au njia nyingine isiyo salama.
1.4 Uhifadhi wa mafuta kwa namna hiyo ni hatari kwa Usalama, Afya na Mazingira. Ni dhahiri kuna matukio mengi ya moto ambayo yamesababishwa na uhifadhi wa mafuta majumbani au kwenye vibanda vya biashara. Ajali hizo za moto, zimegharimu maisha ya watu na kuharibu mali. Pia, wafanyabishara katika maeneo hayo wako hatarini kupata magonjwa ya kansa ya ngozi kutokana na kushika mafuta wakati wa kutoa huduma hiyo. Kwa upande mwingine, mafuta humwagika ardhini na kuharibu mazingira.
1.5 Kuhifadhi mafuta kutumia vyombo vya plastiki kunaharibu ubora wa mafuta hayo na hasa mafuta ya petroli. Mafuta na vyombo vya plastiki vina asili moja. Ubora wa mafuta ya petroli pia unaweza kuathiriwa na mwanga wa jua. Hivyo, vyombo vya moto vinavyo tumia mafuta yanayohifadhiwa kwenye vyombo vya plastiki viko hatarini kupata madhara kwa sababu ya kutumia mafuta ambayo hayana ubora unaohitajika.
1.6 Biashara ya mafuta ya petroli ni muhimu sana, lakini ni hatari ikiwa itafanyika kiholela bila kufuata misingi ya usalama na viwango. Hivyo ni vyema mafuta ya petroli yakahifadhiwa na kuuzwa kwenye miundombinu ambayo imetengenezwa kwa ajili ya kazi hiyo. Lengo ni kulinda usalama, afya, ubora wa mafuta na mazingira.
1.7 Moja ya miundombinu ambayo inatimiza lengo tajwa hapo juu ni vituo vya kuuzia mafuta. Sababu kubwa ni kuwa, kwenye kituo cha mafuta, matenki ya kuhifadhia mafuta yanafukiwa chini ya ardhi. Hivyo, hata moto ukitokea si rahisi mafuta yaliyo ndani ya matenki hayo kulipuka.
1.8 Kipeperushi hiki kimelenga kutoa maelezo kwa kifupi juu ya ujenzi wa vituo vya gharama nafuu kwa kuelezea vitu muhimu na vya msingi vinavyotakiwa kuzingatiwa wakati wa kujenga kituo cha mafuta. Vilevile, Kipeperushi hiki kinaelezea Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini ambazo zilitungwa mahsusi kwa ajili ya kupunguza gharama za uwekezaji wa vituo hivyo.
1.9 Ni lengo la EWURA kutengeneza mazingira ambapo watu wa Vijijini wanakuwa na haki sawa na watu wa Mijini katika upatikanaji wa bidhaa ya mafuta kwa hali ya ubora na usalama unaohitajika na kwa bei nafuu.
1.10 Ni matumaini ya EWURA kwamba, Kipeperushi hiki kitatoa mwanga kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa mafuta ya petroli nchini namna ambavyo uwekezaji wa vituo vya mafuta Vijijini unavyoweza kufanywa kwa gharama nafuu na kuwawezesha watumiaji wa mafuta hayo kupata huduma nzuri zaidi na salama bila kumuathiri mfanyabiashara wa mafuta.
2 Mahitaji na Mambo ya Kuzingatia Wakati wa Ujenzi
Ili uweze kujenga kituo unatakiwa kuzingatia yafutatayo:
(a) Uwe na kiwanja ambacho Mamlaka husika (mfano: Halmashauri ya kijiji) imeridhia kitumike kwa ajili ya biashara ya kituo cha mafuta. Ili kukidhi viwango vya usalama (safety distance requirements), kiwanja kinachofaa kujenga kituo cha mafuta kinatakiwa angalau kiwe na ukubwa wa mita za mraba 400.
(b) Uwe angalau na tenki moja (1) la kuhifadhia mafuta. Kama utauza aina zaidi ya moja ya mafuta, matenki yaongezeke sawia. Tenki liwe na ujazo wa angalau lita 4,500 au 5,000.
Uwe na pampu yenye mkono mmoja au miwili kulingana na aina za mafuta.
(c) Bomba nne (4) za chuma za inchi nne (inchi ) na urefu wa mita tano (mita 5) kwa ajili ya kujengea paa (canopy). Pia, utahitaji bomba za inchi moja au inchi 1.5 na bati kwa ajili ya kenchi na kuezeka (angalia Mchoro Na 2). Bomba za kenchi zinatakiwa kuwa na urefu wa mita saba (mita 7).
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia wakati wa ujenzi:
(a) Matenki ya kuhifadhia mafuta inabidi yafukiwe ardhini kwa umakini mkubwa. . Kwa sehemu ambazo maji ya ardhini (water table) yapo karibu, ni vizuri matenki yakajengewa zege.
(b) Matenki yapakwe rangi ya kuzuia kutu. Pia, matenki yanatakiwa yafukiwe na mchanga kwa ajili ya kuzuia kutu.
(c) Kituo kinatakiwa kisakafiwe kwa zege imara la angalau inchi nne (inchi 4). Eneo mahsusi la kusakafia ni eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta (angalia Mchoro Na 1). Eneo linalozunguka pampu liwe na ukubwa wa angalu mita za mraba 45 (yaani upana mita 6.4 na urefu mita 7). Eneo la kushushia mafuta linatakiwa liwe na ukubwa wa angalau mita za mraba 16 (yaani upana mita 4 na urefu mita 4) ili gari la mafuta liweze kusimama kwenye zege hiyo wakati wa kushusha mafuta.
(d) Eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta ijengewe mitaro inayoelekea kwenda kwenye chemba ya kuchuja mafuta na maji (Oil/water separator). Chemba ya kuchuja mafuta na maji inatakiwa iwe na vyumba vitatu. Kila chumba kiwe na urefu wa mita moja (mita 1), upana mita mbili (mita 2) na kina mita moja (mita 1). Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo. Usitumie zege, ili iwe rahisi wakati wa kusafisha (angalia Mchoro Na 3).
(e) Kituo kinatakiwa kiwe na paa imara (canopy) kama inavyoonyesha kwenye Mchoro Na 2. Paa linatakiwa kuwa na urefu wa mita 5.
(f) Ni vyema kutumia wahandisi wa ujenzi au mafundi wenye uzoefu wa ujenzi wa vituo vya mafuta.
3 Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini
EWURA imeandaa Kanuni mahsusi kwa ajili ya ujenzi na biashara ya vituo vya mafuta vijijini. Kwa mujibu wa kanuni hizo, mtu yeyote anayetaka kujenga kituo kijijini ni lazima kabla ya kuanza ujenzi apate kibali cha EWURA, baada ya kutuma maombi ya kupewa kibali hicho. Pia, kabla ya kuanza biashara, mwekezaji anatakiwa kuwa na leseni ya EWURA, ambayo hutolewa baada ya EWURA kupokea maombi yaliyozingatia mahitaji yote. Baada ya hapo, EWURA itakagua kituo husika ili kujiridhisha kuwa kinakidhi viwango.
Mchoro Na 1: Ramani ya Kituo cha mafuta inayoonyesha tenki, pampu, ofisi, barabara ya kuingia na kutoka kituoni.
Mchoro Na 2: Picha ikionyesha paa la kituo (canopy).
.
Mchoro Na 2: Chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator)
Mchoro Na 3: Picha namna chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator) inavyotakiwa kujengwa. Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo.
Ndugu Moses,
Kiasi hicho cha pesa hakitoshi kwa bishara unayotarajia kufanya.
Nakushauri uangali fursa nyingine kama kuwa wakala wa gesi ya kupikia ama vilainishi ili ukuze mtaji kidogo ili uweze kuanzisha hiyo bishara.
Tafadhali pokea kipeperushi katika barua pepe yako kupata maelezo ya uanzishwaji wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini.
Karibu
Umeeleza vizuri vigezo na masharti nimekuelewa lakini mkuu kiwango cha pesa tunahitaji kujua ni shingapi kwa wafanya biashara wadogo wa vituo vya mafuta kwa vijijini ili tuweze kujiwekeza mfano pump shingapi au ujenzi unaghalimu shingapi
Hongera kwa kazi. Je. Ewura mnamikataba ambayo mnaweza ingia na mtu na kumfadhiri hela kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha mafuta(kijiji) . Kama huduma hiyo mnayo naomba ufafanuzi kama hamna pia naomba muongozo ni kina nan wanahusika. Sory reply via dausonbuninange@yahoo.com
Ndugu Dauson,
Tunapenda kukufahamisha kwamba EWURA haitoi huduma hiyo.
Unaweza kujaribu kuwasiliana na wenye makamouni ya mafuta huenda ukapata ufumbuzi.
Karibu.
Naomba kufahamu kwanini kunaongezeko kubwa la vituo vya mafuta katika maeneo ya makazi ya watu Jijini Dar es Salaam. Je, ile hatari ya milipuko na athari zingine kwa mali na maisha ya binadamu hivi sasa haipo tena?
Vituo vingi vilivyojengwa njia ya Kigogo-Ubungo Maziwa, External-Maji Chumvi viko katikati ya makazi ya watu.
Ndugu Edgar,
Vituo vya mafuta hujengwa kwa mujibu wa utaratibu na kabla ya kutoa kibali cha ujenzi, EWURA hujiridhisha kwamba taratibu zote zimezingatiwa. Vilevile, suala la usalama, mazingira na afya huzingatiwa kabla ya kibali husika kutolewa. Vilevile, baada ya kituo kuanza kazi, EWURA hufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kujiridhusha kuwa kanuni za uendeshaji vituo, ubora wa miundombinu na huduma vinazingatiwa.
Ndugu Anthony,
Makadirio ya gharama ni shs milioni 50. inaweza kuongezeka kutokana na masuala mbalimbali. Aidha EWURA imepunguza ada ya leseni kwa asilimia 90 kwa vituo vya kijijini.
Habari naomba kujua,
mtaji shilingi ngapi unahitajika kuanza biashara ya mafuta ya petrol, diesel na kerosene na je ujenzi wa hapa dar es salaam sheli inatakiwa kuwa na kiwango cha shillingi ngapi pia na kwa mkoa wa pwani pia
Ms Harrieth
Ujenzi wa Kituo cha mafuta inategemea eneo na ukubwa wa kituo cha mafuta unachohitaji. Yafuatayo ni masuala zenye gharama katika ujenzi wa kituo cha mafuta:
1. Jengo la ofisi: Hii inategemea ukubwa wa Ofisi itakayojengwa. Quantity Surveyor (QS) anaweza kukupa gharama halisi za ujenzi baada ya kuona mchoro wa ofisi. Suala la msingi kuwe na ofisi na vyoo angalau viwili.
2. Matenki ya kuhifadhi mafuta. Gharama zinategemea ukubwa wa matenki na idadi. Gharama ya tenki inaweza kuanzia Shilingi milioni 12. Lakini ni vyema matenki uyatengeneze (fabrication) kwenye eneo ambalo utajenga kituo.
3. Kujenga zege eneo la kituo (paving with concrete). Hii inategemea ukubwa wa eneo na jinsi eneo lilivyo. Endapo itahijika kusawazisha (levelling) gharama zinaongezeka. Kwa wastani zege inaweza kugharimu Shilingi milioni 30 – 40.
4. Ujenzi wa Paa (canopy) hii inategemea ukubwa wa kanopi. Kwa wastani canopy inaweza kugharimu hadi Shilingi milioni 40-50.
5. Pampu za kuuzia mafuta. Hii inatagemea idadi na aina ya pampu. Gharama ya pampu moja mpya inaweza kuanzia Shilingi milioni 10-15.
Kimsingi hivyo ndio vitu muhimu. Inapaswa kuwaona Wahandisi washauri na QS kwa ajili ya kupata gharama halisi.
habari, naomba kuuliza inachukua mda gani kuomba lesen ya ufundi umeme baada ya kulipia bei ya ada 10,000/=
Inachukua siku 30 za kazi tangu kupokea maombi kamili kupatiwa leseni.
naomba nitumie gharama za kuanzisha kituo cha mafuta
tafadhali , naomba kujua utaratibu wa kufungua kituo cha mafuta
Ndugu William,
Mwombaji yeyote wa leseni ya rejareja ya mafuta, sharti afanye maombi kwa njia ya kieletroniki kupitia http://www.ewura.go.tz/lois. Taarifa muhimu zinazohitajika kuambatanishwa katika maombi hayo ni:
(a) Nakala ya nyaraka za usajili wa Kampuni au Leseni ya Biashara;
(b) Nakala ya Hati Miliki ya kiwanja palipojengwa kituo cha mafuta au uthibitisho
kutoka Mamlaka husika iliyoruhusu ujenzi wa kituo hicho.
(c) Nakala ya kibali cha ujenzi kutoka Halmashauri au Manispaa husika.
(d) Nakala ya Cheti cha Tathmini ya Athari ya Mazingira (Environmental Impact Assessment Certificate) kinachotolewa na Baraza la Hifadhi ya Mazingira.
(e) Nakala ya cheti cha mlipa kodi (TIN Certificate).
(f) Nakala ya cheti cha zima moto (Fire Safety Certificate) kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani.
(g) Kibali cha ujenzi kutoka EWURA (kwa vituo vilivyojengwa baada ya Aprili 2009).
(h) Orodha ya miundombinu iliyopo katika eneo hilo. Kwa upande wa matanki uooneshwe ujazo wake.
(i) Mchoro wa kituo ambao umesainiwa na Mhandisi aliyesajiliwa na Baraza la Wahandisi Tanzania ukionesha yafuatayo:
(i) umbali uliopo kati ya miundombinu ya kituo cha mafuta;
(ii) mahali pa kuingilia na kutokea kituoni;
(iii) mpaka wa kiwanja;
(iv) mahali pampu zinapotegemewa kufungwa; na
(j) Stakabadhi ya malipo ya ada ya maombi ya leseni.
MASHARTI YA KUPEWA LESENI YA REJAREJA YA KUENDESHA BIASHARA YA MAFUTA
Pamoja na kuwasilisha nyaraka zilizotajwa, kituo cha mafuta sharti kikaguliwe ili kuona kama kinakidhi masharti ya kupewa leseni. Masharti hayo ni pamoja na:
(a) Kuwa na vifaa vya kutosha vya kuzimia moto: Angalau ndoo moja ya mchanga na mtungi mmoja wa kilogramu 9 aina ya “ABE” kwa kila eneo ilipo pampu.
(b) Kuwepo switchi ya dharura iliyowekwa sehemu inayoonekana na kufikika kwa urahisi na mtu yeyote kwa ajili ya kuzima umeme. Swichi iandikwe “SWICHI YA DHARURA”.
(c) Kuwepo na vyoo safi na vya kutosha kwa ajili ya wafanyakazi wa kituo na wateja kwa ujumla. Viwepo vyoo vya wanaume na wanawake.
(d) Alama za kutosha za usalama zinazoonekana vizuri na mteja anapoingia hapo kituoni. Alama hizo ni pamoja na: Zima Injini, Zima Simu na Usivute Sigara.
(e) Matanki, vifaa vya kupimia ujazo wa matanki (dip rods) na pampu lazima viwe vimehakikiwa na Wakala wa Vipimo (WMA). Aidha, pampu sharti ziwe katika hali nzuri ya kufanya kazi.
(f) Mifuniko ya sehemu ya kushushia mafuta na pampu sharti iandikwe ili kuonesha aina ya mafuta yaliyomo au yanayouzwa.
(g) Mifuniko ya matanki ya mafuta sharti ipakwe rangi zifuatazo: Petroli – Nyekundu, Dizeli – Njano na Mafuta ya taa – Bluu
(h) Kila mfuniko wa tanki na mahali pa kuteremshia mafuta vitengenezwe kulingana na viwango vinavyokubalika katika tasnia ya mafuta.
(i) Kituo kiwe kimesakafiwa kwa zege angalau mita nne (4) kuzunguka maeneo yote ya pampu na mahali pa kushushia mafuta na pia kiwe na mfereji uliojengwa vizuri na unaoungana na kitenganisha maji na mafuta (oil/water separator).
(j) Kitenganisha maji na mafuta sharti kiwe na vyumba (chemba) vitatu na kila chumba kiwe na urefu usiopungua mita 1, upana wa mita 2 na kimo cha mita 1. Pia, sharti kiwe na mfuniko unaoweza kufunguliwa kwa urahisi na kuwekwa vali ya kufunga na kufungua mahali pa kutolea maji safi.
(k) Kila tanki la mafuta liwe limeunganishwa na bomba la kupumulia (vent pipe) lenye kimo kisichopungua mita 3.5. Bomba hizo ziwe angalau mita 1.5 kutoka jengo lolote na angalau mita 4.5 kutoka chanzo chochote cha kuingiza hewa au kusababisha moto kama vile dirisha, kiyoyozi, jenereta n.k.
(l) Eneo la pampu liwe limejengewa vizuizi vya kukinga pampu zisigongwe na gari (crush barriers). Vizuizi hivyo viwe na kimo kisichopungua mita moja kutoka sakafu ya kituo.
(m) Kituo kiwe kimejengewa paa (canopy) linalokidhi viwango vinavyotakiwa katika ujenzi wa vituo vya mafuta. Kimo cha paa kisipungue mita 5 na upana wa mita 3 kila upande kutoka katikati ya pampu.
(n) Kituo kiwe katika hali ya usafi.
(o) Kuwepo kwa waya wa kuzuia mwako wa umeme (spark) ambao unaunganishwa na gari la mafuta wakati wa kuteremsha mafuta.
Kituo cha mafuta kinachokidhi masharti tajwa hapo juu, ndicho hupewa leseni na EWURA. Vituo vya mafuta ambavyo havikidhi masharti ya kupewa leseni, haviruhusiwi kufanya biashara hadi hapo vitakapokuwa vimekidhi masharti yote.
ADA NA MUDA WA UHAI WA LESENI
Ada ya leseni ni Shillingi milioni moja (1.000.000/=). Muda wa leseni ni miaka mitano (5). Baada ya uhai wa leseni, mwenye kituo anatakiwa aombe kuhuisha leseni kwa kujaza fomu ya maombi na kuileta EWURA.
Asante.
naomba kujua bei ya resen ya contract
Ndugu Mohamed,
Gharama ya leseni inaazia sh. 20,000/ hadi 150,000/ kulingana na daraja husika.Madaraja ya leseni ni kuanzia w hadi A.
Karibu.
Naomba kujua kama ninaweza kufungua kituo cha kuuza mafuta kwa kuuza bidhaa ya aina moja tu?
Ndugu Yovin,
Unaweza kufanya hivyo.
Karibu
Habari ninaomba kujua utaratibu wa kufungua kituo kidogo cha mafuta kijiji
Ndugu Elihuruma,
Tafadhali rejea barua pepe yako.
Karibu
Nataka kujenga kituo kijijini taratibu zimekaaje?
Ndugu Michael,
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako. Endapo utakuwa na swali au kuhitaji ufafanuzi zaidi, piga simu BURE 0800110030 au andika barua pepe info@ewura.go.tz.
Vilevile unaweza kufika katika Ofisi zetu za makao makuu Dodoma au Kanda zilizopo Arusha, Dar es Salaam, Mbeya,Mwanza na Kanda ya Kati Dodoma.
Karibu.
Naomba kupata taratibu pia za kufungua kituo kidogo cha mafuta vijijini
Habari,nahitaji kujua sifa ya Kila daraja la leseni ya umeme
Ndugu Paulo,
MADARAJA YA LESENI ZA UMEME YANAYOTOLEWA NA EWURA
Leseni Daraja A: inatolewa ili kufanya kazi za umeme katika msongo wa aina zote isipokuwa kazi zilizoruhusiwa chini ya daraja “S1, S2 na S3”.
Leseni Daraja B: inatolewa ili kufanya kazi za umeme mpaka msongo wa kati (33,000V) isipokuwa kazi zilizoruhusiwa chini ya daraja “S1, S2 na S3”.
Leseni Daraja C: inatolewa ili kufanya kazi za umeme mpaka msongo wa chini (400V) isipokuwa kazi zilizoruhusiwa chini ya daraja “S1, S2 na S3”.
Leseni Daraja D: inatolewa ili kufanya kazi za umeme katika msongo wa njia moja (230V) isipokuwa kazi zilizoruhusiwa chini ya daraja “S1, S2 na S3”.
Leseni Daraja W: inatolewa ili kuweza kufanya kazi za ufungaji mifumo ya umeme chini ya usimamizi wa mwenye leseni Daraja A, B, C au D.
Leseni Daraja “S1”: inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme katika msongo wa umeme wa aina zote.
Leseni Daraja “S2”: inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme mpaka msongo wa volti 33,000; na
Leseni Daraja “S3”: inatolewa ili kufanya kazi maalum za ufungaji mifumo ya umeme mpaka msongo wa volti 1,000.
Inabidi kuwe na utofauti wa kilomiter au mita ngapi baina ya kituo na kituo wilayani au mijin ili uweze kufungua kituo kipya?
Ndugu Ali,
Umbali wa kituo na kituo ni mita 200.
Karibu
Naomba kujua ghalama za kuanzisha kituo kido cha mafuta vijijni
Ndugu Samson,
Tafadhali pitia maelezo yafuatayo kwa ufafanuzi zaidi:-
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
1. Utangulizi
1.1 Mahitaji ya mafuta ya petroli na dizeli maeneo ya vijijini yanazidi kuongezeka. Ongezeko hili linatokana na kushamiri kwa shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na usafiri wa pikipiki maarufu kama “boda boda”.
1.2 Hata hivyo, maeneo mengi ya vijijini hayana vituo vya mafuta kutokana na ukweli kwamba, wawekezaji wa biashara hiyo wenye mitaji mikubwa husita kujenga vituo vya kuuzia mafuta Vijijini kwa kuona maeneo hayo hakuna biashara ya kutosha .
1.3 Matokeo yake, wafanyabiashara wenye mitaji midogo na wasio na uzoefu katika biashara ya mafuta, huingia kwenye biashara hii. Kutokana na mitaji yao midogo na kutokuwa na uzoefu, wafanyabiashara hawa huanza kufanya biashara ya mafuta kwa kutumia miundo mbinu hafifu na isiyo salama kama vile kuhifadhi mafuta kwenye mapipa, madumu ya plastiki na kuyauza kwa kutumia chupa za plastiki au njia nyingine isiyo salama.
1.4 Uhifadhi wa mafuta kwa namna hiyo ni hatari kwa Usalama, Afya na Mazingira. Ni dhahiri kuna matukio mengi ya moto ambayo yamesababishwa na uhifadhi wa mafuta majumbani au kwenye vibanda vya biashara. Ajali hizo za moto, zimegharimu maisha ya watu na kuharibu mali. Pia, wafanyabishara katika maeneo hayo wako hatarini kupata magonjwa ya kansa ya ngozi kutokana na kushika mafuta wakati wa kutoa huduma hiyo. Kwa upande mwingine, mafuta humwagika ardhini na kuharibu mazingira.
1.5 Kuhifadhi mafuta kutumia vyombo vya plastiki kunaharibu ubora wa mafuta hayo na hasa mafuta ya petroli. Mafuta na vyombo vya plastiki vina asili moja. Ubora wa mafuta ya petroli pia unaweza kuathiriwa na mwanga wa jua. Hivyo, vyombo vya moto vinavyo tumia mafuta yanayohifadhiwa kwenye vyombo vya plastiki viko hatarini kupata madhara kwa sababu ya kutumia mafuta ambayo hayana ubora unaohitajika.
1.6 Biashara ya mafuta ya petroli ni muhimu sana, lakini ni hatari ikiwa itafanyika kiholela bila kufuata misingi ya usalama na viwango. Hivyo ni vyema mafuta ya petroli yakahifadhiwa na kuuzwa kwenye miundombinu ambayo imetengenezwa kwa ajili ya kazi hiyo. Lengo ni kulinda usalama, afya, ubora wa mafuta na mazingira.
1.7 Moja ya miundombinu ambayo inatimiza lengo tajwa hapo juu ni vituo vya kuuzia mafuta. Sababu kubwa ni kuwa, kwenye kituo cha mafuta, matenki ya kuhifadhia mafuta yanafukiwa chini ya ardhi. Hivyo, hata moto ukitokea si rahisi mafuta yaliyo ndani ya matenki hayo kulipuka.
1.8 Kipeperushi hiki kimelenga kutoa maelezo kwa kifupi juu ya ujenzi wa vituo vya gharama nafuu kwa kuelezea vitu muhimu na vya msingi vinavyotakiwa kuzingatiwa wakati wa kujenga kituo cha mafuta. Vilevile, Kipeperushi hiki kinaelezea Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini ambazo zilitungwa mahsusi kwa ajili ya kupunguza gharama za uwekezaji wa vituo hivyo.
1.9 Ni lengo la EWURA kutengeneza mazingira ambapo watu wa Vijijini wanakuwa na haki sawa na watu wa Mijini katika upatikanaji wa bidhaa ya mafuta kwa hali ya ubora na usalama unaohitajika na kwa bei nafuu.
1.10 Ni matumaini ya EWURA kwamba, Kipeperushi hiki kitatoa mwanga kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa mafuta ya petroli nchini namna ambavyo uwekezaji wa vituo vya mafuta Vijijini unavyoweza kufanywa kwa gharama nafuu na kuwawezesha watumiaji wa mafuta hayo kupata huduma nzuri zaidi na salama bila kumuathiri mfanyabiashara wa mafuta.
2 Mahitaji na Mambo ya Kuzingatia Wakati wa Ujenzi
Ili uweze kujenga kituo unatakiwa kuzingatia yafutatayo:
(a) Uwe na kiwanja ambacho Mamlaka husika (mfano: Halmashauri ya kijiji) imeridhia kitumike kwa ajili ya biashara ya kituo cha mafuta. Ili kukidhi viwango vya usalama (safety distance requirements), kiwanja kinachofaa kujenga kituo cha mafuta kinatakiwa angalau kiwe na ukubwa wa mita za mraba 400.
(b) Uwe angalau na tenki moja (1) la kuhifadhia mafuta. Kama utauza aina zaidi ya moja ya mafuta, matenki yaongezeke sawia. Tenki liwe na ujazo wa angalau lita 4,500 au 5,000.
Uwe na pampu yenye mkono mmoja au miwili kulingana na aina za mafuta.
(c) Bomba nne (4) za chuma za inchi nne (inchi ) na urefu wa mita tano (mita 5) kwa ajili ya kujengea paa (canopy). Pia, utahitaji bomba za inchi moja au inchi 1.5 na bati kwa ajili ya kenchi na kuezeka (angalia Mchoro Na 2). Bomba za kenchi zinatakiwa kuwa na urefu wa mita saba (mita 7).
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia wakati wa ujenzi:
(a) Matenki ya kuhifadhia mafuta inabidi yafukiwe ardhini kwa umakini mkubwa. . Kwa sehemu ambazo maji ya ardhini (water table) yapo karibu, ni vizuri matenki yakajengewa zege.
(b) Matenki yapakwe rangi ya kuzuia kutu. Pia, matenki yanatakiwa yafukiwe na mchanga kwa ajili ya kuzuia kutu.
(c) Kituo kinatakiwa kisakafiwe kwa zege imara la angalau inchi nne (inchi 4). Eneo mahsusi la kusakafia ni eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta (angalia Mchoro Na 1). Eneo linalozunguka pampu liwe na ukubwa wa angalu mita za mraba 45 (yaani upana mita 6.4 na urefu mita 7). Eneo la kushushia mafuta linatakiwa liwe na ukubwa wa angalau mita za mraba 16 (yaani upana mita 4 na urefu mita 4) ili gari la mafuta liweze kusimama kwenye zege hiyo wakati wa kushusha mafuta.
(d) Eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta ijengewe mitaro inayoelekea kwenda kwenye chemba ya kuchuja mafuta na maji (Oil/water separator). Chemba ya kuchuja mafuta na maji inatakiwa iwe na vyumba vitatu. Kila chumba kiwe na urefu wa mita moja (mita 1), upana mita mbili (mita 2) na kina mita moja (mita 1). Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo. Usitumie zege, ili iwe rahisi wakati wa kusafisha (angalia Mchoro Na 3).
(e) Kituo kinatakiwa kiwe na paa imara (canopy) kama inavyoonyesha kwenye Mchoro Na 2. Paa linatakiwa kuwa na urefu wa mita 5.
(f) Ni vyema kutumia wahandisi wa ujenzi au mafundi wenye uzoefu wa ujenzi wa vituo vya mafuta.
3 Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini
EWURA imeandaa Kanuni mahsusi kwa ajili ya ujenzi na biashara ya vituo vya mafuta vijijini. Kwa mujibu wa kanuni hizo, mtu yeyote anayetaka kujenga kituo kijijini ni lazima kabla ya kuanza ujenzi apate kibali cha EWURA, baada ya kutuma maombi ya kupewa kibali hicho. Pia, kabla ya kuanza biashara, mwekezaji anatakiwa kuwa na leseni ya EWURA, ambayo hutolewa baada ya EWURA kupokea maombi yaliyozingatia mahitaji yote. Baada ya hapo, EWURA itakagua kituo husika ili kujiridhisha kuwa kinakidhi viwango.
Mchoro Na 1: Ramani ya Kituo cha mafuta inayoonyesha tenki, pampu, ofisi, barabara ya kuingia na kutoka kituoni.
Mchoro Na 2: Picha ikionyesha paa la kituo (canopy).
.
Mchoro Na 2: Chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator)
Mchoro Na 3: Picha namna chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator) inavyotakiwa kujengwa. Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo.
Nashukuru kwa maelezo mazuri ya kufungua au kuanziasha kituo cha mafuta vijijini.
Naomba kupata kipeperushi
Naomba kipeperushi hiki kwenye email christian.dondo@yahoo.com hapa sijaweza kuona picha
Almost makadilio kama tsh ngap kinaweza kukamilika kituo hicho
Ndugu Simon,
Kituo cha mafuta maeneo ya vijijini vinakadiriwa kugharimu kati ya milioni 50-70. Hata hivyo gharama inaweza kubadilika kutokana na masuala mbalimnali ikiwemo gharama za malighafi. Vituo vya mijini gharama yake inategemea na ukubwa wa kituo
Karibu
Kufungua kituo wilayani au mijini inabidi kuwepo na utofauti wa kilomiter ngap au mita ngapi baina ya kituo nakituo?
kuomba kituo cha kuuza mafuta tunaombaje
Ndugu Nigo,
Hatua ya awali ni kufanya maombi ya kibali cha ujenzi kupitia mtandao katika mfumo uitwao LOIS, kwenye tovuti yetu.
Karibu.
je ada yakulipia ili kupata lesen ni shngap?
Bwana Tito,
Ada ya maombi ni tsh 10,000/ na malipo ya leseni inategemea na daraja lako la leseni, kiwango cha juu kabisa ni tsh 120,000/ kwa daraja A. Na inaendelea kushuka mpaka kufikia wiremen. Nakushauri upitie Kanuni za Ufungaji meme za mwaka 2019, zilizopo katika tovuti yetu, ukurusa wa Umeme.
Kwa maelezo zaidi piga simu bure 0800110030
Karibu
Nahitaji kipeperush kwa vijijini
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Nawapongeza kwa Kazi bora mnayoifanya kwa muujibu wa
Maelezo yenu mtandaoni.
Habari
Mara nyingi tunajua bei ya petrol inavouzwa ila inakonunuliwa napataje kujua bei zake kwa kila msimu je natumia website gan kujua au link ipi au nifanyaje nipate kujua bei ya manunuzi
Ndugu Joseph, ununuzi wa mafuta yanayotumika nchini hufanywa kwa pamoja kwa uratibu wa Wakala ya Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA) na mafuta hununuliwa katika soko la dunia. Pitia https://www.pbpa.go.tz/ ili uweze kupata taarifa zaidi.
Karibu
Bwana Lugoe,
Ada ya leseni ni Shillingi milioni moja (1.000.000/=). Na muda wa leseni ni miaka mitano (5).
Kumbuka:- Maombi ya leseni hufanyika kwa njia ya mtandao kupitia kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Kwa maelezo zaidi piga 0800110030.
Karibu
Tafadhali naomba nipate utaratibu mzima wa kufungua kituo kidogo cha mafuta mikoani(vijijini) ikijumuisha na gharama zote muhimu zinazohitajika
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
naomba kujua utaratibu wa kufungua kituo cha mafuta kijijini focusmawe@gmail.com
Ndugu Focus, utaratibu umetumwa katika barua pepe yako.
Karibu
Naomba pia utalatibu wa kufungua kituo cha mafuta.
Ndugu Edgar,
Tafadhali rejea barua pepe yako.
Karibu
Nimepata taarifa kuwa Ewura mmerahisisha taratibu za kujenga kituo cha mafuta kijijini kwa gharama nafuu tofauti na mjini. Naomba kujua vi vitu gani vya kuzingatia ili niweze kuwekeza kituo cha mafuta vijijini.
Habari Sammy,
Nakutumia kipeperushi kwa email ukipitie. Endapo utakuwa na swali lolote usisite kuwasiliana nasi. Pia unaweza kupiga simu bure kwa namba 0800110030
Please nitumie Taratibu za kujenga kituo cha mafuta mjini na vijiji. Tumia email hii mtafya05@gmail.com
Nami naomba nipatiwe utaratibu wa kufungua sheli ndogondogo vijijini
Nahitaji kujua taratibu za kufungua kituo Cha mafuta yaan Petro station kijijin
Email yangu ni henryjane49@gmail.com
Tafadhali naomba kujua taratibu zake
Ndugu Jane,
Tafadhali, utaratibu umetumwa katika barua pepe yako.
Karibu
Nami naitaji mnipe mwongozo mzuma wa kufungua kituo kidogo cha mafuta ikiwa ni petrol tuu
Ndugu Gerald,
Mwongozo huo ufuatao:-
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
1. Utangulizi
1.1 Mahitaji ya mafuta ya petroli na dizeli maeneo ya vijijini yanazidi kuongezeka. Ongezeko hili linatokana na kushamiri kwa shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na usafiri wa pikipiki maarufu kama “boda boda”.
1.2 Hata hivyo, maeneo mengi ya vijijini hayana vituo vya mafuta kutokana na ukweli kwamba, wawekezaji wa biashara hiyo wenye mitaji mikubwa husita kujenga vituo vya kuuzia mafuta Vijijini kwa kuona maeneo hayo hakuna biashara ya kutosha .
1.3 Matokeo yake, wafanyabiashara wenye mitaji midogo na wasio na uzoefu katika biashara ya mafuta, huingia kwenye biashara hii. Kutokana na mitaji yao midogo na kutokuwa na uzoefu, wafanyabiashara hawa huanza kufanya biashara ya mafuta kwa kutumia miundo mbinu hafifu na isiyo salama kama vile kuhifadhi mafuta kwenye mapipa, madumu ya plastiki na kuyauza kwa kutumia chupa za plastiki au njia nyingine isiyo salama.
1.4 Uhifadhi wa mafuta kwa namna hiyo ni hatari kwa Usalama, Afya na Mazingira. Ni dhahiri kuna matukio mengi ya moto ambayo yamesababishwa na uhifadhi wa mafuta majumbani au kwenye vibanda vya biashara. Ajali hizo za moto, zimegharimu maisha ya watu na kuharibu mali. Pia, wafanyabishara katika maeneo hayo wako hatarini kupata magonjwa ya kansa ya ngozi kutokana na kushika mafuta wakati wa kutoa huduma hiyo. Kwa upande mwingine, mafuta humwagika ardhini na kuharibu mazingira.
1.5 Kuhifadhi mafuta kutumia vyombo vya plastiki kunaharibu ubora wa mafuta hayo na hasa mafuta ya petroli. Mafuta na vyombo vya plastiki vina asili moja. Ubora wa mafuta ya petroli pia unaweza kuathiriwa na mwanga wa jua. Hivyo, vyombo vya moto vinavyo tumia mafuta yanayohifadhiwa kwenye vyombo vya plastiki viko hatarini kupata madhara kwa sababu ya kutumia mafuta ambayo hayana ubora unaohitajika.
1.6 Biashara ya mafuta ya petroli ni muhimu sana, lakini ni hatari ikiwa itafanyika kiholela bila kufuata misingi ya usalama na viwango. Hivyo ni vyema mafuta ya petroli yakahifadhiwa na kuuzwa kwenye miundombinu ambayo imetengenezwa kwa ajili ya kazi hiyo. Lengo ni kulinda usalama, afya, ubora wa mafuta na mazingira.
1.7 Moja ya miundombinu ambayo inatimiza lengo tajwa hapo juu ni vituo vya kuuzia mafuta. Sababu kubwa ni kuwa, kwenye kituo cha mafuta, matenki ya kuhifadhia mafuta yanafukiwa chini ya ardhi. Hivyo, hata moto ukitokea si rahisi mafuta yaliyo ndani ya matenki hayo kulipuka.
1.8 Kipeperushi hiki kimelenga kutoa maelezo kwa kifupi juu ya ujenzi wa vituo vya gharama nafuu kwa kuelezea vitu muhimu na vya msingi vinavyotakiwa kuzingatiwa wakati wa kujenga kituo cha mafuta. Vilevile, Kipeperushi hiki kinaelezea Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini ambazo zilitungwa mahsusi kwa ajili ya kupunguza gharama za uwekezaji wa vituo hivyo.
1.9 Ni lengo la EWURA kutengeneza mazingira ambapo watu wa Vijijini wanakuwa na haki sawa na watu wa Mijini katika upatikanaji wa bidhaa ya mafuta kwa hali ya ubora na usalama unaohitajika na kwa bei nafuu.
1.10 Ni matumaini ya EWURA kwamba, Kipeperushi hiki kitatoa mwanga kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa mafuta ya petroli nchini namna ambavyo uwekezaji wa vituo vya mafuta Vijijini unavyoweza kufanywa kwa gharama nafuu na kuwawezesha watumiaji wa mafuta hayo kupata huduma nzuri zaidi na salama bila kumuathiri mfanyabiashara wa mafuta.
2 Mahitaji na Mambo ya Kuzingatia Wakati wa Ujenzi
Ili uweze kujenga kituo unatakiwa kuzingatia yafutatayo:
(a) Uwe na kiwanja ambacho Mamlaka husika (mfano: Halmashauri ya kijiji) imeridhia kitumike kwa ajili ya biashara ya kituo cha mafuta. Ili kukidhi viwango vya usalama (safety distance requirements), kiwanja kinachofaa kujenga kituo cha mafuta kinatakiwa angalau kiwe na ukubwa wa mita za mraba 400.
(b) Uwe angalau na tenki moja (1) la kuhifadhia mafuta. Kama utauza aina zaidi ya moja ya mafuta, matenki yaongezeke sawia. Tenki liwe na ujazo wa angalau lita 4,500 au 5,000.
Uwe na pampu yenye mkono mmoja au miwili kulingana na aina za mafuta.
(c) Bomba nne (4) za chuma za inchi nne (inchi ) na urefu wa mita tano (mita 5) kwa ajili ya kujengea paa (canopy). Pia, utahitaji bomba za inchi moja au inchi 1.5 na bati kwa ajili ya kenchi na kuezeka (angalia Mchoro Na 2). Bomba za kenchi zinatakiwa kuwa na urefu wa mita saba (mita 7).
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia wakati wa ujenzi:
(a) Matenki ya kuhifadhia mafuta inabidi yafukiwe ardhini kwa umakini mkubwa. . Kwa sehemu ambazo maji ya ardhini (water table) yapo karibu, ni vizuri matenki yakajengewa zege.
(b) Matenki yapakwe rangi ya kuzuia kutu. Pia, matenki yanatakiwa yafukiwe na mchanga kwa ajili ya kuzuia kutu.
(c) Kituo kinatakiwa kisakafiwe kwa zege imara la angalau inchi nne (inchi 4). Eneo mahsusi la kusakafia ni eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta (angalia Mchoro Na 1). Eneo linalozunguka pampu liwe na ukubwa wa angalu mita za mraba 45 (yaani upana mita 6.4 na urefu mita 7). Eneo la kushushia mafuta linatakiwa liwe na ukubwa wa angalau mita za mraba 16 (yaani upana mita 4 na urefu mita 4) ili gari la mafuta liweze kusimama kwenye zege hiyo wakati wa kushusha mafuta.
(d) Eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta ijengewe mitaro inayoelekea kwenda kwenye chemba ya kuchuja mafuta na maji (Oil/water separator). Chemba ya kuchuja mafuta na maji inatakiwa iwe na vyumba vitatu. Kila chumba kiwe na urefu wa mita moja (mita 1), upana mita mbili (mita 2) na kina mita moja (mita 1). Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo. Usitumie zege, ili iwe rahisi wakati wa kusafisha (angalia Mchoro Na 3).
(e) Kituo kinatakiwa kiwe na paa imara (canopy) kama inavyoonyesha kwenye Mchoro Na 2. Paa linatakiwa kuwa na urefu wa mita 5.
(f) Ni vyema kutumia wahandisi wa ujenzi au mafundi wenye uzoefu wa ujenzi wa vituo vya mafuta.
3 Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini
EWURA imeandaa Kanuni mahsusi kwa ajili ya ujenzi na biashara ya vituo vya mafuta vijijini. Kwa mujibu wa kanuni hizo, mtu yeyote anayetaka kujenga kituo kijijini ni lazima kabla ya kuanza ujenzi apate kibali cha EWURA, baada ya kutuma maombi ya kupewa kibali hicho. Pia, kabla ya kuanza biashara, mwekezaji anatakiwa kuwa na leseni ya EWURA, ambayo hutolewa baada ya EWURA kupokea maombi yaliyozingatia mahitaji yote. Baada ya hapo, EWURA itakagua kituo husika ili kujiridhisha kuwa kinakidhi viwango.
Mchoro Na 1: Ramani ya Kituo cha mafuta inayoonyesha tenki, pampu, ofisi, barabara ya kuingia na kutoka kituoni.
Mchoro Na 2: Picha ikionyesha paa la kituo (canopy).
.
Mchoro Na 2: Chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator)
Mchoro Na 3: Picha namna chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator) inavyotakiwa kujengwa. Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo.
Bwana Sammy karibu.
Ni kweli. Tafadhali tupatie anuani ya barua pepe ili upate kipeperushi chenye maelezo husika.
Karibu
Naomba na mimi unipatie kipeperushi kwa ajili ya kuanzisha sheli . silascos@gmail.com
Bwana Silas,
Sawa.
Karibu
Naomba na Mimi nipate kipeperushi cha uanzishaji kituo cha mafuta kijijini
henrykisinda@gmail.com
Ndugu Henry,
Tafadhali pitia katika barua pepe yako kusoma kipeperushi.
na Mimi pia naomba kipeperushi ni namna gani nitaanza biashara ya shell na gharama zake asanteni sana
Bi Theresia, ni vituo vya mafuta sio shell.
Tafadhali kipeperushi kimetumwa katika baraua pepe yako.
Karibu
Nahitaji kipeperushi kituo kidogo cha mafuta vijijini, nitumie kwemye email: zawuya@gmail.com
Namimi naombeni
obedidamasi9@gmail.com
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Naomba kujua taratibu za kufungua KITUO kidogo cha kuuza mafuta.
Na mimi pia nahitaji kipeperushi
kimarocharles960@gmail.com
Naoma na Mimi nakala ya kipeperushi abubakaritarimo.aht@gmail.com
Ndugu Abubakari,
Tfadhali angalia katika barua pepe yako.
Asante
Hello, nami naomba kutumiwa kipeperushi
avinpeter1994@gmail.com
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako. Karibu
NAOMABA NA MIMI UNITUMIE KIPEPERUSHI HICHO KATIKA EMAIL paschaljames00@gmail.com
na mimi naomba ekihwili400@gmail.com
Pamoja na garama ya ada na leseni ki ujumla na ushuru ili nipate jiandaa vyema
Ndugu Gerald,
Gharama ya maombi ya leseni ni shilingi 10,000/
Ada ya leseni inatofautiana kwa aina ya leseni kuanzia shilingi 40,000 mpaka 150,000/
Ada zote hudumu kwa muda wa miaka mitatu.
Asante
Tafadhali na mimi naomba nakala ya kipeperushi cha kufuata ili kufungua kituo cha mafuta kijijini ,
Asante
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Tafadhali na mimi naomba nakala ya kipeperushi cha kufuata ili kufungua kituo cha mafuta kijijini ,
Asante
Tafadhali na mimi naomba nakala ya kipeperushi cha kufuata ili kufungua kituo cha mafuta kijijini ,
Asante.
sangarichard802@gmail.com
Ndugu Richard,
Tafadhali angalia katika barua pepe yako.
Karibu
Hello.
Lubricants Wholesale Business Licence inachukua mda gani mpaka kukamilika ikiwa documents zote ziko kamili?
Bwana Kijika,
Leseni hutolewa ndani ya siku 30 za kazi baada ya kupokea maombi kamili. Endapo una suala au changamoto yoyote wasiliana nasi na unaweza kupiga simu bure 0800110030.
Karibu
Bwana Kijika,
Kwa mujibu wa mkataba wetu wa huduma, Leseni hutolewa ndani ya siku 30 za kazi tangu tarehe ya kupokea maombi yaliyo kamili.
Karibu
Naomba mnitumie taratibu za kuanzisha kituo cha mafuta kidogo vijijini
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Inakuaje mtu anaomba lesen ya umeme daraja C mnampa daraja D wakati kazi zake nying ni 3phese
Habari, ningependa kujua utaratibu na documents zinazotumika kuomba kibali au leseni ya kufanya biashara ya kuuza vilainishi/ lubricants kwa kampuni. Kama kuna kipeperushi tafadhali naomba nisaidiwe.
Asante
Ndugu Makota,
Utaratibu unaotumika ni kufanya maombi kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa kieletroniki kwa kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/.
Pia pitia ukurasa huu https://www.ewura.go.tz/approval-and-licencing/ kwa maelezo zaidi.
Pia tutumie email yako tafadhali.
Na unaweza kupiga simu 0800110030 (bure) kwa maelezo zaidi au ufafanuzi.
Karibu
Naomba kujua garama za kuanzisha kituo kidogo cha mafuta nalenga boda boda na baadhi ya magari kwa upande wa vijijini.maana nimesikia kuna gharama kidogo nafuu.
Ndugu Kafyome,
Tfadhali,makadirio ya gharama ni takribani milioni 55. Hata hivyo gahrama hii inaweza kuzidi kidogo au kupungua kwa sababu mbalimbali.
Naomba utume anuani yako ya barua pepe ili tukutumie maelezo husika.
Asante
Josephalbinus@gmail.com
Naomba na Mimi ubitumie kipeperushi ndugu
Sawa.
Naomba kutumiwa kipeperushi cha Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta vijijini
Naomba na mimi kipeperushi chenye maelekezo
Naomba na mimi unitumie kipeperushi cha kuanza kituo cha mafuta kijijini
Maombi hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu na kubofya LOIS, kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako.
Nitumie mwongozo kwenye barua pepe hii
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Tafadhali naomba kupata makadirio ya uanzishaji wa kituo kidogo cha mafuta kijijini na utaratibu wake. Nalenga watu wa bodaboda na magari pia mashine za kusaga.
Email yangu ni jsumni@gmail.com
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki— https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Karibu
Naomba nitumiwe kipeperushi kwa e mail yangu
Ndugu Rivnus,
Umetumiwa katika barua pepe yako.
Karibu.
Naomba na Mimi kipeperushi domiciancrecencia@gmail.com
Hellow ewura ,
Good job,ina eneo langu njia ya kuelekea msumi mbezi DSM ina mapango wa kujenga kituo cha mafuta.naomba kufahamishwa taratibu za kuanza kujenga Hadi nafungua kituo .thanks
Good job
Ndugu Mlay,
Karibu
Tafadhali angalia barua pepe maelezo ya utaratibu yametumwa kwa rejea yako.
Asante
naomba kujua utaratibu za kufungua petro station vijijini
Bwana Wambura.
Tafadhali anagalia barua pepe yako kwa mwongozo.
Asante
Tafadhari naomba msaada mchanganuo wa gharama za kuanzisha kituo kidogo Cha mafuta(shell)
Habari za Asubuhi
Hongereni kwa kazi kubwa mnayofanya
Naomba kuuliza: Nina mpango kwa kuanzisha Kituo Kidogo cha Mafuta au pump kwa ajili ya kuhudumia watu wa Kijijini kwani Sheli zipo mbali. Naomba kupata utaratibu ili niweze kujua kama nitaweza.
Karibu Ndugu Kalinga,
Tafadhali mwongozo umetumwa katika baraua pepe yako.
Asante
Habari za asubuhi
Nahitaji kipeperushi kituo kidogo cha mafuta vijijini
Asante
Bwana Kadari,
Rejea katika barua pepe yako.
Karibu.
Naomba kipeperushi jinsi ya kufungua kituo kidogo cha mafuta kisarawe pwani
Habari, Ewura kulikuwa na mpango wa kuanza kutoa vibali kwa ajili ya uanzishwaji wa mobile petrol station (Guta Petrol Station) haswa kwa maeneo ya vijijini. Tafadhali naweza kupata maelezo zaidi juu ya utolewaji wa leseni ya vituo hivyo vya mafuta na taratibu za kufuatwa. Na je Fuel dispenser ya aina yoyote inaweza kutumika katika uuzaji wa mafuta au kuna aina za dispenser ndio zinazokidhi vigezo?. Na naomba kupata kipeperushi cha uanzishaji wa kituo cha mafuta vijijini.
email masaganya07@hotmail.com
Ndugu George,
Utaratibu wa vituo tembezi (mobile petrol stations) bado haujakamilika. Utakapokuwa tayari au vinginevyo taarifa itatolewa. Kuhusu kipeperushi,tafadhali rejea ktk barua pepe yako.
Kwa maelezo zaidi piga 080011030 BURE
Asante
Hello habari Ewura
Niko interested na kupata maelezo ya kuwa na hizi mobile fuel station, na pia hiyo namba ambayo ni ya huduma kwa mteja haipatikani. tunaomba msaada zaidi
Pia namimi naomba kupata nakala ya maelezo ya hizo petrol station ndogo vijijini.
habari nilikua nauliza eneo la ukubwa gani linalohitajika kwa ujenzi wa kituo cha mafuta
Ndugu Mohamed,
Ukubwa wa eneo inategemea aina ya kituo na mahali kinapojengwa. Kwa maeneo ya vijini ni kuanzia mita za mraba 400.
Kwa maelezo zaidi tupigie 0800110030 bila gaharama.
Karibu
Naomba kipeperushi cha leseni za umeme kulingana na class. Email: brianhelp175@gmail.com
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Kipeperushi kimetumwa katika barua pepe yako. Karibu
Nahitaj kipeperushi kituo kidogo cha mafuta vijijini
ni umbali gani unatakiwa baina ya kituo cha mafuta sheli na makazi ya watu
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Habari,
Naomba kujua utaratibu wa kujenga mpaka kufungua kituo cha mafuta kwa Dar es salaam na mkoani.
Asante.
Ndugu Jane,
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako. Utaratibu huu unatumika ni kwa maeneo yote. Tofauti ni katika aina ya kituo na eneo linalohtajika. Kwa maeneo ya Dar es Salaam, ukubwa wa eneo ni kuanzia sq 1500 mpaka 2400.
Aidha, Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Karibu.
Naomba kuuliza ukitaka kuanzisha utoaji wa mafuta katika maeneo Ya kijijini vigezo vikoje na gharama zake zikoje?
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Je naweza kupata utaratibu wa kufungua kituo cha mafuta kwa vijijini
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako
Habari Ewura, niko kwenye utafiti wa gharama za kujenga kituo cha mafuta mjini , gharama zisiuhusishe eneo. Nimejaribu kutafuta mwenyewe nimepata majibu mchanganyiko. Naomba msaada tafadhari.
Ndugu James,
Hongera kwa kazi hiyo.
Tunashauri utupatie majibu mchanganyiko uliyopata ili tuweze kubaini endapo umepata majibu sahihi ama la.
Hata hivyo, Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Tafadhali naomba kipeperushi cha vituo vidogo vya mafuta vijijini
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Tafadhali naomba nipate utaratibu mzima wa kufungua kituo kidogo cha mafuta mikoani(vijijini) ikijumuisha na gharama zote muhimu zinazohitajika
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.wura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Naomba kipeperushi chenye utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta vijijini. Niliomba hapo kabla kwenye uzi wa mtu mwingine. Pia kama utaratibu wa kuuza kwa kutumia guta/kirikuu kama umekamilika tafadhali ambatanisha vipeperushi vyote. Asante
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako.
Utaratibu wa vituo tembezi bado haujakamilika. Karibu
Habari za asubuhi.
Nahitaji kipeperushi kituo cha mafuta
Habari, ulishajibiwa.
Habari za asubuhi
Nahitaji kipeperushi kuhusu taratibu za kuanzisha kituo cha mafuta maeneo ya mjini.
Email yangu jumanneathuman@gmail.com
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako. Karibu
Naomba kipeperushi cha kuanzisha kituo cha mafuta kijijini. Email yangu ni Lmdendemi@gmail.com
Asante.
Maombi ya leseni hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu http://www.ewura.go.tz; kisha bofya LOIS kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Maelezo ya utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta umetumwa katika barua pepe yako. Karibu
Habari za leo Muheshimiwa, Eweru ningependa kupata information zozote kuhusu kufungua kituo cha mafuta mjini na kijijini pia. Ikiwa nchini au nchini jirani hususani nchi toka Maziwa Makuu. Na nijinsi gani pia mnaweza kusaidia kufanikisha swala la ufunguaji kituo cha mafuta.
Maombi hufanyika kupitia mfumo wa kieletroniki unaitwa LOIS.Tafadhali ingia katika website yetu na kubofya LOIS, kujisajili na kuendelea kufanya maombi. Unaweza pia kutumia kiunganishi hiki—https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako.
Na mimi naomba kipeperushi kweny email yangu nkuba03stephen@gmail.com
Ndugu Nkuba,
Umetumiwa.
Karibu
Mimi nipo nyumba ya mungu, Simanjiro, naomba muongozo wa hatua ninazopaswa kufuata ninapotaka kufungua kituo cha mafuta, napenda kujua procedures na gharama za ada za serikali. Tayari nimeshachimba visima vya kuweka matanki
Ndugu Festo,
Tupatie namba yako ya simu tafadhali.
Karibu
Naomba nitumie kipeperushi cha utaratibu wa kufungua filling station kijijin
eliascharles@live.com
Hata mm nahtaji kujua taratbu za kujenga kituo cha mafuta kijijin naomba msaaada wa maelekezo na gharama zpo vp
Habari.
Tafadhali naomba kupatiwa utaratibu wa kupata lesini ya uuzaji wa mafuta ya petroli na dizeli kwa njia ya mobile (yaani kuuza mafuta bila kua na kituo cha mafuta yaani kwa kutumia gari yenye tenki na pampu)
Habari naomba kupata kipeperushi na maelezo kuhusu kuanzisha sheli johntuju94@gmail.com
Habari, Naomba msaada mchanganuo wa gharama katika kuanzisha kituo Cha mafuta (sheli)
Habari,
Nimeomba Construction approval kwa ajili ya kituo caha mafuta , nimefuatilia hatua na kuona ipo hatua ya Review and Approval , je baada ya hatua io kuna hatua zaidi , na kama zipo bado ngapi hadi kuweza kupata kibari cha ujenzi !
Asante
Sanga .
Habari Team EWURA.
Napenda kujua taratibu /muongozo kamili wa Kuanzisha kituo cha mafuta kiwe kidogo,cha kati au kikubwa mjini au kijijini,ili kuona ni wapi naweza jikita.
Ahsanteni.
Email: muhsinmustaph@yahoo.co.uk
Habari team EWURA.
Mimi ni mdau wa sekta ya mafuta.Napenda kufahamu sasa muongozo kamili na gharama za kuanzisha kituo cha mafuta kwa mjini na ama kijijini kiwe kikubwa au kidogo.
Nitashkuru ombo langu likifanyiwa kazi na kupata majibu
Tafadhali naomba kipeperushi email yang hiyo
Naomba kutumiwa kipeperushi nmna ya kufungua kituo vijijini. Email-ikhalfan18@gmail.com
Naomba kipeperushi namna ya Kufungua Kituo Cha Mafuta Vijijini . Email-ikhalfan18@gmail.com
Tafadhali naomba kujua jinsi ya kufungua kituo cha mafuta , gharama zote pamoja na vigezo. zanzibar Tanzania
Ewura naomba mnitumie kipeperushi namna ya Kufungua Kituo Cha Mafuta Vijijini . Email-ikhalfan18@gmail.com
Habari, ninaitwa Nelson tafadhali naomba kujua taratibu za kufuata pamoja na ada husika ili kuweza kupata kibali cha kuuza mafuta (yaani petroli na dizeli) kwa njia ya mobile (kwa kutumia gari zenye tanki zilizofungwa pampu). Asante.
Naomba kipeperushi cha kituo kidogo cha mafuta vijijin
Habari
Naomba kipeperushi Cha utaratibu wa kufungua kituo cha mafuta. Kwenye email hii gbalibaza77@gmail.com
Naomba kipeperushi cha kuanzisha kituo cha mafuta kijijini.
naomba kipeperushi cha gharama za uanzilishaji wa kituo cha mafuta. Email yangu ni Stanleymuza68@gmail.com
Habari kiongozi naweza pata muongozo wa wauzaji mafuta wadogo na wanahitajika kukamilisha vitu gani ili waweze kupata leseni ya biashara hiyo
Habari,
Nahitaji kuwa mfanya biashara wa mafuta (liquid)vijijini je naweza kupata mwangaza wa pa kuanzia,na naomba kupata vipeperushi vinavyotoa miongozo email yangu ni hakimusadock@gmail.com
Tafadhali naomba Maelezo ya Utaratibu wa Kuanzisha Kituo cha Mafuta
Nathamini na kuheshimu kazi nzuri ambazo EWURA imekuwa ikifanya kwa maendeleo ya Taiga letu. Naomba nisaidiwe kipeperushi cha kufahamu namna ya uanzishaji na ufunguaji wa kituo cha mafuta vijijini.
Naomba kupatiwa kipeperushi cha taratibu za kufungua kituo cha mafuta mjini na vijijini
Naomba kipeperushi Cha maelekezo ya kuanzisha kituo Cha Mafuta kijijini. Na Kama naweza kupata makadirio ya gharama za uanzishaji. Nahitaji Sana.
habari
naomba kutumiwa kipeperushi cha kuanzisha kituo cha mafuta kijijini na mjini. Email yangu ni idd19mussa@gmail.com
Ndugu Idd,
Kipeperushi imetumwa katika barua pepe yako.
Karibu.
Na Mimi nitumie kipeperushi mpendwa email sirgdabraza@gmail.com
umbali gani unatakiwa kisheria mtu anapojenga kituo cha mafuta kwenywe makazi ya watu?
Naomba kujua utaratibu wa vituo vya mafuta kuuziana mafuta kwa mujibu wa sheria umekaaje naomba msaada hilo jambo.
Ndugu Alson, vituo vya mafuta kuuziana mafuta haina tatizo kwa sababu ni maelewano yao. Jambo la msingi ni kuhakikisha katika kufanya hivyo hawavunji sheria. Hata hivyo ni kwa mujibu wa Kifungu cha 26(2)(b)(ii) cha Kanuni za Bidhaa za Mafuta (Jumla, Rejareja, Kuhifadhi na Matumizi Binafsi),Tangazo la Serikali Na . 817 la mwaka 2020, kila mmoja anapaswa kuingia mkataba wa mauziano ya mafuta na wauzaji wa mafuta kwa ujumla.
Karibu
Hongera kwa kazi. Naomba kipeperushi cha utaratibu wakuanzisha kituo cha mafuta.
Habari
Naomba kufahamu gharama za kufungua kituo kidogo cha mafuta kijijini/vijijini.
Hongera kwa kazi. Naomba kipeperushi cha utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta
Hongera kwa kazi. Naomba kipeperushi cha utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta kwenye
manfredmlowe@gmail.com
Habari za leo, naomba kupewa utaratibu wa kuanzisha na kusajili kituo cha uuzaji mafuta (petrol na diesel) kijijini. Ingekuwa vyema nikaelekezwa hatua ya kwanza mpaka ya mwisho ikiwa tayari nina eneo ambalo ndilo natarajia kulitumia kwa shughuli/biashara hiyo. Pamoja na uwanja huu ni vyema nipewe majibu kwa barua pepe yangu. Asante
ME NAITAJI KUANZISHA KITUO CHA MAFUTA NA JE NITARATIBU GANI NAFUATA
Tafadhali na mimi naomba nakala ya kipeperushi cha kufuata ili kufungua kituo cha mafuta kijijini ,
Asante
email yangu ni fmlaki@gmail.com
Ndugu Frank,
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako.
Karibu
Hello
Nahitaji kuanzisha kituo Kidogo cha mafuta (Mini Petrol Station) Kigoma vijijini. Nisaidieni hatua za kufuata, sample bajeti structure, kusajili na kupata leseni
Ndugu Mawazo,
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako.
Endapo utahitaji taarifa zaidi usisiste kuwasiliana nasi.
Karibu
Naomba nipate utaratibu wa kuanzisha kituo cha mafuta
Ndugu Michael,
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako, hata hivyo, maeneo ya vijijini na mijini ni ukubwa wa eneo ambao kwa mjini ni mita za mraba 1200 hadi 2400 kulingana na aina ya kituo kinachokusudiwa kujengwa.
Endapo utahitaji taarifa zaidi usisiste kuwasiliana nasi.
Karibu
habari za leo,
Ninalo eneo ambalo ningependa kufungua kituo cha kuuzia mafuta na spear parts.
Hivyo naomba kujua utaratibu kuanzia mwanzo hadi mwisho pamoja na gharama zake. Eneo lipo pugu dar es salaam
Ndugu Jacquiline,
Utaratibu umetumwa katika barua pepe yako, hata hivyo, maeneo ya vijijini na mijini ni ukubwa wa eneo ambao kwa mjini ni mita za mraba 1200 hadi 2400 kulingana na aina ya kituo kinachokusudiwa kujengwa.
Endapo utahitaji taarifa zaidi usisiste kuwasiliana nasi.
Karibu
Habari, naomba kufahamu kuna maeneo yanahesabika yapo mjini lakini kiuhalisia ni kijijini kabisa. Kwa mfano kayenze mwanza. Inahesabika iko ndani ya manispaa ya ilemela lakini kwa waopajua ni kijijini kabisa. Hapo inakaaje kuhusu lile swala la leseni zenu za kurahisisha huduma kwa wanakijiji kama hao? Masharti yatabaki yale yale kama ya kituo cha mjini?
Ndugu Jaffar
Ilemela yote ni mjini. Kwa ufafanuzi zaidi kuhusu maeneo husika fika ofisi za Manispaa.
Karibu
Naomba kujua, ni umbali gani unaopaswa kuwepo baina ya kituo kimoja na kingine.
Ndugu Tumikiaeli,
Ni mita 200.
Asante
Naomba kupata kipeperushi chenye kuonesha masharti na vigezo vya kuanzisha kituo Cha mafuta vijijini
Ndugu Samwel,
Pokea kama ifuatavyo:-
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
UJENZI WA VITUO VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
1. Utangulizi
1.1 Mahitaji ya mafuta ya petroli na dizeli maeneo ya vijijini yanazidi kuongezeka. Ongezeko hili linatokana na kushamiri kwa shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na usafiri wa pikipiki maarufu kama “boda boda”.
1.2 Hata hivyo, maeneo mengi ya vijijini hayana vituo vya mafuta kutokana na ukweli kwamba, wawekezaji wa biashara hiyo wenye mitaji mikubwa husita kujenga vituo vya kuuzia mafuta Vijijini kwa kuona maeneo hayo hakuna biashara ya kutosha .
1.3 Matokeo yake, wafanyabiashara wenye mitaji midogo na wasio na uzoefu katika biashara ya mafuta, huingia kwenye biashara hii. Kutokana na mitaji yao midogo na kutokuwa na uzoefu, wafanyabiashara hawa huanza kufanya biashara ya mafuta kwa kutumia miundo mbinu hafifu na isiyo salama kama vile kuhifadhi mafuta kwenye mapipa, madumu ya plastiki na kuyauza kwa kutumia chupa za plastiki au njia nyingine isiyo salama.
1.4 Uhifadhi wa mafuta kwa namna hiyo ni hatari kwa Usalama, Afya na Mazingira. Ni dhahiri kuna matukio mengi ya moto ambayo yamesababishwa na uhifadhi wa mafuta majumbani au kwenye vibanda vya biashara. Ajali hizo za moto, zimegharimu maisha ya watu na kuharibu mali. Pia, wafanyabishara katika maeneo hayo wako hatarini kupata magonjwa ya kansa ya ngozi kutokana na kushika mafuta wakati wa kutoa huduma hiyo. Kwa upande mwingine, mafuta humwagika ardhini na kuharibu mazingira.
1.5 Kuhifadhi mafuta kutumia vyombo vya plastiki kunaharibu ubora wa mafuta hayo na hasa mafuta ya petroli. Mafuta na vyombo vya plastiki vina asili moja. Ubora wa mafuta ya petroli pia unaweza kuathiriwa na mwanga wa jua. Hivyo, vyombo vya moto vinavyo tumia mafuta yanayohifadhiwa kwenye vyombo vya plastiki viko hatarini kupata madhara kwa sababu ya kutumia mafuta ambayo hayana ubora unaohitajika.
1.6 Biashara ya mafuta ya petroli ni muhimu sana, lakini ni hatari ikiwa itafanyika kiholela bila kufuata misingi ya usalama na viwango. Hivyo ni vyema mafuta ya petroli yakahifadhiwa na kuuzwa kwenye miundombinu ambayo imetengenezwa kwa ajili ya kazi hiyo. Lengo ni kulinda usalama, afya, ubora wa mafuta na mazingira.
1.7 Moja ya miundombinu ambayo inatimiza lengo tajwa hapo juu ni vituo vya kuuzia mafuta. Sababu kubwa ni kuwa, kwenye kituo cha mafuta, matenki ya kuhifadhia mafuta yanafukiwa chini ya ardhi. Hivyo, hata moto ukitokea si rahisi mafuta yaliyo ndani ya matenki hayo kulipuka.
1.8 Kipeperushi hiki kimelenga kutoa maelezo kwa kifupi juu ya ujenzi wa vituo vya gharama nafuu kwa kuelezea vitu muhimu na vya msingi vinavyotakiwa kuzingatiwa wakati wa kujenga kituo cha mafuta. Vilevile, Kipeperushi hiki kinaelezea Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini ambazo zilitungwa mahsusi kwa ajili ya kupunguza gharama za uwekezaji wa vituo hivyo.
1.9 Ni lengo la EWURA kutengeneza mazingira ambapo watu wa Vijijini wanakuwa na haki sawa na watu wa Mijini katika upatikanaji wa bidhaa ya mafuta kwa hali ya ubora na usalama unaohitajika na kwa bei nafuu.
1.10 Ni matumaini ya EWURA kwamba, Kipeperushi hiki kitatoa mwanga kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa mafuta ya petroli nchini namna ambavyo uwekezaji wa vituo vya mafuta Vijijini unavyoweza kufanywa kwa gharama nafuu na kuwawezesha watumiaji wa mafuta hayo kupata huduma nzuri zaidi na salama bila kumuathiri mfanyabiashara wa mafuta.
2 Mahitaji na Mambo ya Kuzingatia Wakati wa Ujenzi
Ili uweze kujenga kituo unatakiwa kuzingatia yafutatayo:
(a) Uwe na kiwanja ambacho Mamlaka husika (mfano: Halmashauri ya kijiji) imeridhia kitumike kwa ajili ya biashara ya kituo cha mafuta. Ili kukidhi viwango vya usalama (safety distance requirements), kiwanja kinachofaa kujenga kituo cha mafuta kinatakiwa angalau kiwe na ukubwa wa mita za mraba 400.
(b) Uwe angalau na tenki moja (1) la kuhifadhia mafuta. Kama utauza aina zaidi ya moja ya mafuta, matenki yaongezeke sawia. Tenki liwe na ujazo wa angalau lita 4,500 au 5,000.
Uwe na pampu yenye mkono mmoja au miwili kulingana na aina za mafuta.
(c) Bomba nne (4) za chuma za inchi nne (inchi ) na urefu wa mita tano (mita 5) kwa ajili ya kujengea paa (canopy). Pia, utahitaji bomba za inchi moja au inchi 1.5 na bati kwa ajili ya kenchi na kuezeka (angalia Mchoro Na 2). Bomba za kenchi zinatakiwa kuwa na urefu wa mita saba (mita 7).
Yafuatayo ni mambo ya kuzingatia wakati wa ujenzi:
(a) Matenki ya kuhifadhia mafuta inabidi yafukiwe ardhini kwa umakini mkubwa. . Kwa sehemu ambazo maji ya ardhini (water table) yapo karibu, ni vizuri matenki yakajengewa zege.
(b) Matenki yapakwe rangi ya kuzuia kutu. Pia, matenki yanatakiwa yafukiwe na mchanga kwa ajili ya kuzuia kutu.
(c) Kituo kinatakiwa kisakafiwe kwa zege imara la angalau inchi nne (inchi 4). Eneo mahsusi la kusakafia ni eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta (angalia Mchoro Na 1). Eneo linalozunguka pampu liwe na ukubwa wa angalu mita za mraba 45 (yaani upana mita 6.4 na urefu mita 7). Eneo la kushushia mafuta linatakiwa liwe na ukubwa wa angalau mita za mraba 16 (yaani upana mita 4 na urefu mita 4) ili gari la mafuta liweze kusimama kwenye zege hiyo wakati wa kushusha mafuta.
(d) Eneo linalozunguka pampu na eneo la kushushia mafuta ijengewe mitaro inayoelekea kwenda kwenye chemba ya kuchuja mafuta na maji (Oil/water separator). Chemba ya kuchuja mafuta na maji inatakiwa iwe na vyumba vitatu. Kila chumba kiwe na urefu wa mita moja (mita 1), upana mita mbili (mita 2) na kina mita moja (mita 1). Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo. Usitumie zege, ili iwe rahisi wakati wa kusafisha (angalia Mchoro Na 3).
(e) Kituo kinatakiwa kiwe na paa imara (canopy) kama inavyoonyesha kwenye Mchoro Na 2. Paa linatakiwa kuwa na urefu wa mita 5.
(f) Ni vyema kutumia wahandisi wa ujenzi au mafundi wenye uzoefu wa ujenzi wa vituo vya mafuta.
3 Kanuni za EWURA za ujenzi wa vituo vijijini
EWURA imeandaa Kanuni mahsusi kwa ajili ya ujenzi na biashara ya vituo vya mafuta vijijini. Kwa mujibu wa kanuni hizo, mtu yeyote anayetaka kujenga kituo kijijini ni lazima kabla ya kuanza ujenzi apate kibali cha EWURA, baada ya kutuma maombi ya kupewa kibali hicho. Pia, kabla ya kuanza biashara, mwekezaji anatakiwa kuwa na leseni ya EWURA, ambayo hutolewa baada ya EWURA kupokea maombi yaliyozingatia mahitaji yote. Baada ya hapo, EWURA itakagua kituo husika ili kujiridhisha kuwa kinakidhi viwango.
Mchoro Na 1: Ramani ya Kituo cha mafuta inayoonyesha tenki, pampu, ofisi, barabara ya kuingia na kutoka kituoni.
Mchoro Na 2: Picha ikionyesha paa la kituo (canopy).
.
Mchoro Na 2: Chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator)
Mchoro Na 3: Picha namna chemba ya kuchuja mafuta na Maji (Oil/Water Separator) inavyotakiwa kujengwa. Chemba ifunikwe na mifuniko iliyotengenezwa na bati au kichanja imara kilichotegenezwa na nondo.
Nahitaj kipeperushi kituo kidogo cha mafuta vijijini
Nahitaj kipeperushi kituo kidogo cha mafuta vijijini
naomba kufahamu bei ya malipo ya ya kupata leseni ya Biashara ya mafuta ya petroli kama Retail au ni Class gani.Ahsante
Ndugu Mudhihiri,
Gharama ya leseni ni 1,000,000/
Habari!nahitaji kufahamu yakuwa biashara ya mafuta ya Retail Leseni yake ni CLASS GANI?
Ndugu Mudhihiri,
Leseni za biashara ya bidhaa za petroli hutolewa kwa aina ya biashara na si kwa daraja.
Asante
mafuta ya PETROL
Nina milioni 8 kwenye akaunti! Ninaweza kuanzia kituo cha kuuzia mafuta-petrol tu hapa kijijini kwetu? Naomba msaada.
Ndugu Moses,
Kiasi hicho cha pesa hakitoshi kwa bishara unayotarajia kufanya.
Nakushauri uangali fursa nyingine kama kuwa wakala wa gesi ya kupikia ama vilainishi ili ukuze mtaji kidogo ili uweze kuanzisha hiyo bishara.
Tafadhali pokea kipeperushi katika barua pepe yako kupata maelezo ya uanzishwaji wa vituo vya mafuta maeneo ya vijijini.
Karibu
Umeeleza vizuri vigezo na masharti nimekuelewa lakini mkuu kiwango cha pesa tunahitaji kujua ni shingapi kwa wafanya biashara wadogo wa vituo vya mafuta kwa vijijini ili tuweze kujiwekeza mfano pump shingapi au ujenzi unaghalimu shingapi
Ndugu Herzon,
Kipeperushi kimeanisha mchanganuo wa makadirio ya gharama.
Karibu
Hongera kwa kazi. Je. Ewura mnamikataba ambayo mnaweza ingia na mtu na kumfadhiri hela kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha mafuta(kijiji) . Kama huduma hiyo mnayo naomba ufafanuzi kama hamna pia naomba muongozo ni kina nan wanahusika. Sory reply via dausonbuninange@yahoo.com
Ndugu Dauson,
Tunapenda kukufahamisha kwamba EWURA haitoi huduma hiyo.
Unaweza kujaribu kuwasiliana na wenye makamouni ya mafuta huenda ukapata ufumbuzi.
Karibu.
Naomba kufahamu kwanini kunaongezeko kubwa la vituo vya mafuta katika maeneo ya makazi ya watu Jijini Dar es Salaam. Je, ile hatari ya milipuko na athari zingine kwa mali na maisha ya binadamu hivi sasa haipo tena?
Vituo vingi vilivyojengwa njia ya Kigogo-Ubungo Maziwa, External-Maji Chumvi viko katikati ya makazi ya watu.
Mamlaka zinazohusika zinasubiri maafa gani?
Ndugu Edgar,
Vituo vya mafuta hujengwa kwa mujibu wa utaratibu na kabla ya kutoa kibali cha ujenzi, EWURA hujiridhisha kwamba taratibu zote zimezingatiwa. Vilevile, suala la usalama, mazingira na afya huzingatiwa kabla ya kibali husika kutolewa. Vilevile, baada ya kituo kuanza kazi, EWURA hufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kujiridhusha kuwa kanuni za uendeshaji vituo, ubora wa miundombinu na huduma vinazingatiwa.
Karibu
Almost inaweza kugharimu kiasi gani kwa kituo cha kijijini? Kukamilisha kituo cha petrol pekee
Nahitaji pdf nzima ya hatuavza kufuata ili kuanzisha kituo Cha mafuta mjini au vijijini. Full pdf document
Nami nataka kujua hili swala
Ndugu Ditra,
Tafadhali tembelea barua pepe yako, maelezo yametumwa.
Karibu
Naomba kipeperushi kinacho eleza utaratibu wa kufungua vituo vya mafuta vijijini
Ndugu Daniel,
Tunapenda kukufahamisha kwamba kipeperushi kimetumwa kwenye barua pepe yako.
Karibu
habari,
naomba kujua umbali kutoka kituo kinapojengwa na makazi ya watu
Hongera EWURA kwa kazi nzuri, naomba kipeperushi kinachohusu UJENZI WA VITUO VYA VYA KUUZIA MAFUTA REJAREJA VYA GHARAMA NAFUU – VIJIJINI
Ndugu Nicetas,
Kipeperushi kimetumwa kwenye barua pepe yako.
Karibu
Samahani gharama za makadirio ya kuanzisha kituo cha mafuta kijijini ni kama vile shingapi?
Ndugu Anthony,
Makadirio ya gharama ni shs milioni 50. inaweza kuongezeka kutokana na masuala mbalimbali. Aidha EWURA imepunguza ada ya leseni kwa asilimia 90 kwa vituo vya kijijini.
Karibu
Naomba nipate kipeperushi Cha kufungua kituo kidogo Cha mafuta ya taa
Ndugu Victoria,
Kipeperushi kimetumwa kwenye barua pepe yako.
Asante
Naomba Kujua Utaratibu wa kupata kibali cha kufungua kituo cha Mafuta (Sheli) kwa upande wa vijijin au semi-town. Na Gharama zake zipoje
Ndugu,
Alex pokea kupitia barua pepe yako
Hello
Naomba kipeperushi cha kufungua kituo kidogo cha mafuta kijiji
Ndugu Jonathan,
Pokea kwenye barua oepe yako.
Habari
Naomba kipeperushi chenye maelekezo ya kujenga kuanzisha kituo cha mafuta kijijini.
Ndugu Herbert,
Umetumiwa kipeperushi kwenye barua pepe.
Karibu
Habari naomba kujua,
mtaji shilingi ngapi unahitajika kuanza biashara ya mafuta ya petrol, diesel na kerosene na je ujenzi wa hapa dar es salaam sheli inatakiwa kuwa na kiwango cha shillingi ngapi pia na kwa mkoa wa pwani pia
Ms Harrieth
Ujenzi wa Kituo cha mafuta inategemea eneo na ukubwa wa kituo cha mafuta unachohitaji. Yafuatayo ni masuala zenye gharama katika ujenzi wa kituo cha mafuta:
1. Jengo la ofisi: Hii inategemea ukubwa wa Ofisi itakayojengwa. Quantity Surveyor (QS) anaweza kukupa gharama halisi za ujenzi baada ya kuona mchoro wa ofisi. Suala la msingi kuwe na ofisi na vyoo angalau viwili.
2. Matenki ya kuhifadhi mafuta. Gharama zinategemea ukubwa wa matenki na idadi. Gharama ya tenki inaweza kuanzia Shilingi milioni 12. Lakini ni vyema matenki uyatengeneze (fabrication) kwenye eneo ambalo utajenga kituo.
3. Kujenga zege eneo la kituo (paving with concrete). Hii inategemea ukubwa wa eneo na jinsi eneo lilivyo. Endapo itahijika kusawazisha (levelling) gharama zinaongezeka. Kwa wastani zege inaweza kugharimu Shilingi milioni 30 – 40.
4. Ujenzi wa Paa (canopy) hii inategemea ukubwa wa kanopi. Kwa wastani canopy inaweza kugharimu hadi Shilingi milioni 40-50.
5. Pampu za kuuzia mafuta. Hii inatagemea idadi na aina ya pampu. Gharama ya pampu moja mpya inaweza kuanzia Shilingi milioni 10-15.
Kimsingi hivyo ndio vitu muhimu. Inapaswa kuwaona Wahandisi washauri na QS kwa ajili ya kupata gharama halisi.
Karibu.