Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), inatangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli hapa nchini. Bei hizi zitaanza kutumika kuanzia Alhamisi, Tarehe 1 Julai 2021 ili kuendana na na Sheria ya Fedha ya Mwaka 2021 na mabadiliko mengine ya sheria ambayo yataanza kutumika ifikapo tarehe 1 Julai 2021. Mabadiliko yanayohusu bidhaa za petroli kama yalivobainishwa katika Sheria ya Fedha ya Mwaka 2021 na mabadiliko mengine ya sheria ni: (i) ongezeko la tozo ya mafuta kwa shilingi 100 kwa kila lita moja ya mafuta ya petroli na dizeli na (ii) kuongezeka kwa ada ya petroli kwa shilingi 100 kwa kila lita moja ya mafuta ya taa.
Soma Zaidi:-https://www.ewura.go.tz/fuel-prices/
Hits: 10774
Kinachonishangaza nchi hii ni ubambikiaji wa kodi zisizo za lazima, kwenye bei ya mafuta tunakatwa karibu kodi 3 , VAT, REA na sijui Railway. huu si uungwana kabisa.
Mfano angalia wenzetu Zambia, mpaka sasa bei ya petroleum ni 1800/= Tzs kwa hela ya kwetu Tanzania wakati hayo hayo mafuta yanapakuliwa kutoka Bandari ya hapa kwetu na kusafirishwa mpaka kwao lakini bado wanauza bei ya chini kuliko sisi tatizo ni nini?.
Maudhui mazuri! Endelea na kazi nzuri!
Mafuta ya taa hakuna huku Songea,tunayategemea kupikia,tunaomba mtuletee tunapata tabu.
Maisha yanazid kuwa magumu kwakupanda bei za mafuta kwa upande wetu wahusika wa magari tunaomba nauli zipande jmn😔