TAARIFA inatolewa kwa mafundi wa umeme na umma kwa ujumla kuwa, ni kosa kisheria kufanya kazi za kuweka mifumo ya umeme (electrical installations) bila kuwa na leseni hai iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).
ONYO hili linatolewa kwa mujibu wa Ibara ya 7 (1) ya Sheria ya EWURA namba 414 na Ibara ya 8 ya Sheria ya Umeme namba 131. Soma Zaidi:-
Warning-Electrical Installation Personnel
_____________________________________________________________________________________________________________
Hits: 508
Je tufanyeje sisi tulio na leseni za ufundi umeme ili kupata mhuri na kuweza kupitisha kazi bila kumtegemea kontrakta mwingine asante
Ndugu Manento,
Cha muhimu zaidi ni kujiendeleza kupata elimu ya ngazi ya juu ili upate daraja la leseni linalokuwezesha kuwa na muhuri.Asante.
Je,ni daraja gani la elimu natakiwa kuwa nalo ili kuweza kupewa mhuri?
Ahsante.
Ndugu Masanja,
Unapaswa kuwa na daraja kuanzia wiremen. Na leseni ya kufanya kazi inapatikana kwa kufanya maombi kupitia kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/
Unpaswa kuwa na vyeti vya elimu ya ufundi vilivyothibitishwa, picha (pasipoti) yenye kivuli cha bluu na wasifu wako (CV); vyote vikiwa katika nakala laini kabla ya kuanza kufanya maombi.
Kwa maelezo zaidi piga 0800110030 (bure) au tembelea ofisi yetu iliyo karibu nawe katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma,Mbeya na Mwanza.
Karibu
Mbna Lois system aifun guki
Ndugu Rajabu,
Pole kwa changamoto. Kwa sasa inafunguka.
Endapo utapata tatizo jingine tuma ujumbe support@ewura.go.tz Au piga simu (BURE) 0800110030
Karibu