TAARIFA KWA UMMA: Mwito wa Maoni ya Wadau kuhusu Maombi ya Marekebisho ya Bei za Umeme kutoka Kampumi ya Usambazaji Umeme ya Mwenga kwa Mwaka 2021/22-2023/24

Kwa mujibu wa Kifungu cha 19 (2) (b) cha Sheria ya EWURA, Sura ya 414, kutakuwa na mkutano Jumatatu, tarehe 14 Juni 2021 katika Ukumbi wa Ofisi ya Kijiji cha Igoda Mufindi kuanzia saa 4:00 asubuhi. Lengo kuu la mkutano huo ni kukusanya maoni ya wadau ikiwa ni pamoja na Baraza la Ushauri la Serikali (GCC), Baraza la Ushauri la Watumiaji (CCC), wateja na umma kwa jumla juu ya uhalisia wa maombi ya mabadiliko ya bei zinazopendekezwa.

Soma Zaidi:-

Visits: 338

2 thoughts on “TAARIFA KWA UMMA: Mwito wa Maoni ya Wadau kuhusu Maombi ya Marekebisho ya Bei za Umeme kutoka Kampumi ya Usambazaji Umeme ya Mwenga kwa Mwaka 2021/22-2023/24

    1. Ndugu Hamis,
      Karibu. Maombi ya leseni za umeme hufanyika kwa njia ya mtandao kupitia mfumo wa LOIS unaopatikana katika tovuti ya EWURA.
      Tumia kiunganishi https://lois.ewura.go.tz/ewura/ kujisajili kisha endelea kujaza fomu ya maombi.Unatakiwa kuwa na picha yenye kivuli cha bluu, cheti cha ufundi, kitambulisho na wasifu wako (CV) inayoonesha kazi ulizofanya; vyote vikiwa katika nakala laini (soft copy).
      Endapo utapata changamoto yoyote wasiliana nasi BURE 0800110030 siku na muda wa kazi.
      Karibu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *