EWURA imezindua taarifa ya 15 ya utendaji wa Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanzania bara. Madhumuni ya taarifa hizo ni kuujulisha umma kuhusu hatua iliyofikiwa na mamlaka za maji katika kutoa huduma ya majisafi na usafi wa mazingira, kupima jitihada za mamlaka hizo katika kufikia malengo ya utendaji kazi na kupendekeza hatua za kuboresha utoaji wa huduma. Kwa mwaka 2022/23, amlaka za maji za Iringa, Nzega na Biharamulo ziliibuka vinara katika utoaji wa huduma za majisafi na usafi wa mazingira.
Soma Zaidi:-https://www.ewura.go.tz/sw/utendaji-wa-mamlaka-za-maji-na-usafi-wa-mazingira/
Visits: 1794