Sekta ya Maji na Usafi wa Mazingira

Taarifa za jumla | Shughuli za Udhibiti wa Maji na Usafi wa Mazingira | Nyenzo za Udhibiti wa Maji na Usafi wa Mazingira | Utoaji wa leseniViwango vya bei na tozo  | Masuala ya Afya, Usalama na Mazingira | Ripoti za Utendaji wa Mamlaka za Maji | Utatuzi wa Malalamiko yanayohusu Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira

Taarifa za Jumla

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), ina wajibu wa kudhibiti kiufundi na kiuchumi huduma za maji na usafi wa mazingira.

Mabonde ya maji na huduma za usambazaji maji na usafi wa mazingira, zinaigawanya tasnia ya hii kuwa mbili ambazo ni (i) uangalizi wa raslimali maji ambayo inadhibitiwa na Idara ya Mabonde na, (ii) Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira.

Huduma za Maji na Usafi wa Mazingira hutolewa na Mamlaka za Majisafi na Usafi wa Mazingira, ambazo hudhibitiwa na EWURA. Jumuiya za kijamii za huduma za maji, zinadhibitiwa na Wizara ya Maji kupitia Wakala wa Usambazaji Maji Vijijini (RUWASA).

Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira zimeanzishwa kwa kifungu 91(a) cha sheria ya Majisafi na Usafi wa Mazingira, 2019, ambapo Waziri wa Maji, kwa kushauriana na Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, anaweza kuanzisha Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira kwa kuzingatia vigezo vilivyomo kwenye kanuni ya Usambazaji Maji, 2019 na Notisi ya Serikali Na. 828. Mamlaka za Maji zina wajibu wa kusimamia huduma za usambazaji wa maji na usafi wa mazingira kwenye maeneo ya miji.

Udhibiti wa Maji ulianza mwaka 2006 baada ya marekebisho ya Sheria ya Maji,1949 na Sheria ya Maji na Usafi wa Mazingira, Sura ya 272, ambazo zilianza kufanya kazi Agosti 2009. Kwa sasa udhibiti unafanywa kwa mujibu wa sheria ya Maji na Usafi wa Mazingira, 2019 na Sheria ya EWURA Sura ya 414. Sheria ya Maji na Usafi wa Mazingira inatoa mgawanyo wa majukumu baina ya Wizara ya Maji, Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira na EWURA.

EWURA inazidhibiti takribani mamlaka 94 za maji na usafi wa mazingira ambazo zinahudumia mikoa na makao makuu ya wilaya, miji na miradi ya kitaifa, kama ilivyoonyeshwa kwenye orodha ya mamlaka zinazodhibitiwa hadi kufikia Julai 2020; kama ilivyotangazwa na Waziri mwenye dhamana ya maji kama inavyoainishwa: –

 Orodha ya Mamlaka Zinazodhitiwa na EWURA

Aina ya Mtoa huduma             Idadi ya Watoa huduma

  1. Mamlaka za Mikoa           26
  2. Mamlaka za Miradi ya Maji ya Kitaifa 7
  3. Mamlaka za Wilaya – Zinazojitegemea 25
  4. Mamlaka za Wilaya – Zinazosimamiwa na RUWASA 26
  5. Mamlaka za Wilaya – Zinazosimamiwa na Mamlaka za 10

Jumla ya Mamlaka        94

Miundombinu

Uwezo wa Uzalishaji maji na mahitaji ya huduma ya maji

Kiwango cha uzalishaji majisafi kwa Mamlaka za mikoa na miradi ya kitaifa kwa mwaka 2018/19, kilifikia mita za ujazo milioni 332, ilhali uwezo wa uzalishaji ulifikia mita za ujazo milioni 492, na mahitaji yakiwa mita za ujazo milioni 520. Kwa Mamlaka za Wilaya na Miji Midogo, mwaka 2018/19, kiwango cha uzalishaji wa maji kilifikia mita za ujazo milioni 36.3, wakati mahitaji yalikuwa mita za ujazo milioni 105.3.

Hits: 751